Wednesday, 2 July 2025

MJUMBE MKUTANO MKUU CCM TAIFA,ASIA KINGONGO AMEJITOKEZA KUCHUKUWA NA KURUDISHA FOMU KUWANIA KITI CHA UDIWANI KWAMNDOLWA,,


 

Pichani mkono wa kulia mwanamke ni Mjumbe mkutano mkuu taifa,Mjumbe kamati ya wazazi utekelezaji Mkoa wa Tanga na katibu mwenezi tawi la Kwameta na katibu wa vijana kata ya Kwamndolwa,Asia Ally Kingongo akichukua fomu ya kuwania nafasi ya Udiwani kata ya Kwamndolwa kwa Katibu kata  ya Kwamndolwa iliyopo Korogwe Mjini,Samweli Mbuguje mkono wa kushoto ambaye ni mwanaume.

Picha ni Mjumbe mkutano mkuu CCM taifa,Mjumbe kamati ya wazazi utekelezaji Mkoa wa Tanga na katibu mwenezi wa CCM tawi la Kwameta na katibu wa vijana kata ya Kwamndolwa,Asia Ally Kingongo akichukua fomu ya kuwania nafasi ya Udiwani kata ya Kwamndolwa akionyesha fomu mara baada ya kuchukua nje ya ofisi ya CCM tawi la Kwameta.

Pichani ni Katibu kata  ya Kwamndolwa,Samweli Mbuguje mkono wa kushoto ambaye ni mwanaume.akikagua fomu ya Mjumbe wa mkutano mkuu taifa,Mjumbe kamati ya wazazi utekelezaji Mkoa wa Tanga na katibu Mwenezi CCM tawi la Kwameta na katibu wa vijana kata ya Kwamndolwa,Asia Ally Kingongo alichukua fomu na kurudisha ya kuwania nafasi ya kiti cha Udiwani kata ya Kwamndolwa


Pichani ni Mjumbe wa mkutano Mkuu CCM taifa,Mjumbe kamati ya wazazi Utekelezaji Mkoa wa Tanga na katibu Mwenezi CCM tawi la Kwameta na katibu wa vijana kata ya Kwamndolwa,Asia Ally Kingongo Mara baada ya kuchukua fomu na kurudisha ya kuwania nafasi ya kiti cha Udiwani kata ya Kwamndolwa akiwa na familia yake.

ZOEZI LA MTANGAZAJI WA REDIO UHURU,REHEMA LUSEWA KUCHUKUA NA KURUDISHA FOMU KUWANIA KITI CHA UDIWANI VITI MAALUM ILIKUWA HIVI,,,


Picha mkono wa kulia ni Mjumbe wa baraza la UWT Korogwe Mji na Mtangazaji nguli wa ITV na Uhuru redio ya chama cha Mapinduzi CCM,Rehema Lusewa akichukua fomu ya kuwania nafasi ya Udiwani viti maalum Korogwe mjini kwa Katibu wa UWT Korogwe mjini,Suzan Mandia (mkono wa kulia). 


Picha mkono wa kulia ni Mjumbe wa baraza la UWT Korogwe Mji na Mtangazaji nguli wa ITV na Uhuru redio ya chama cha Mapinduzi CCM,Rehema Lusewa akirudisha fomu ya kuwania nafasi ya Udiwani viti maalum Korogwe mjini kwa Katibu wa UWT Korogwe mjini,Suzan Mandia (mkono wa kulia). 

Picha mkono wa kulia ni Mjumbe wa baraza la UWT Korogwe Mjini na Mtangazaji nguli wa ITV na Uhuru redio ya chama cha Mapinduzi CCM,Rehema Lusewa akisaini mara baada ya kurudisha.






Sunday, 29 June 2025

CHRISTINA AJITOKEZA KUCHUKUWA FOMU KUWANIA NAFASI YA UDIWANI VITI MAALUM,,,


 Picha mkono wa kulia ni Christina Fransis Kabelwa akichukua fomu ya kuwania nafasi ya Udiwani Viti maalum Korogwe vijijini kwa Katibu wa UWT Korogwe vijijini,Nuru Jacob Mwaibako.

ZOEZI LA SHEKAONEKA KUCHUKUA FOMU KUWANIA KITI CHA UBUNGE KOROGWE VIJIJINI LILIKUWA HIVI,,,,,,,

Picha ni Mwenyekiti mstaafu wa UVCCM mkoa wa Mbeya mjini na Katibu elimu malezi na mazingira mkoa wa Mbeya,Ramadhani Mahmud Shekaoneka akichukua fomu kuwania nafasi ya Ubunge kwa Karibu wa CCM wilaya ya Korogwe vijijini,Safina Alfred Nchinbi ambaye ni (mwanamke mkono wa kushoto). 

 


Picha ni Mwenyekiti mstaafu wa UVCCM mkoa wa Mbeya mjini na Katibu elimu malezi na mazingira mkoa wa Mbeya,Ramadhani Mahmud Shekaoneka akisaini mara baada ya kuchukua fomu kuwania nafasi ya Ubunge.
Picha ni Mwenyekiti mstaafu wa UVCCM mkoa wa Mbeya mjini na Katibu elimu malezi na mazingira mkoa wa Mbeya,Ramadhani Mahmud Shekaoneka akichukua mara baada ya kuchukua fomu kuwania nafasi ya Ubunge nje ya ofisi hizi akionyeshwa kwa wasindikizaji wake.


Picha ni Mwenyekiti mstaafu wa UVCCM mkoa wa Mbeya mjini na Katibu elimu malezi na mazingira mkoa wa Mbeya,Ramadhani Mahmud Shekaoneka akichukua mara baada ya kuchukua fomu kuwania nafasi ya Ubunge nje ya ofisi hizi akionyeshwa kwa wasindikizaji wake na.akiwa na miongoni mwa wasindikizaji wake.


Picha  Mwenyekiti mstaafu wa UVCCM mkoa wa Mbeya mjini na Katibu elimu malezi na mazingira mkoa wa Mbeya,Ramadhani Mahmud Shekaoneka mara baada ya kuchukua fomu kuwania nafasi ya Ubunge akipewa maelekezo na taratibu za chama hicho kwa Katibu wa CCM wilaya ya Korogwe vijijini,Safina Alfred Nchinbi ambaye ni (mwanamke mkono wa kushoto). 


Picha ni Mwenyekiti Mstaafu wa UVCCM mkoa wa Mbeya mjini na Katibu elimu malezi na mazingira mkoa wa Mbeya,Ramadhani Mahmud Shekaoneka mara baada ya kuchukua fomu kuwania nafasi ya Ubunge akipewa maelekezo na taratibu za chama hicho kwa Katibu wa CCM wilaya ya Korogwe vijijini.


ZOEZI LA KUCHUKUA FOMU LILIKUWA HIVI,,,AMINA MAGOGO AJITOKEZA KUWANIA NAFASI YA UBUNGE JIMBO LA KOROGWE VIJIJINI,,

Picha mkono wa kulia ni Amina Magogo akipokea fomu ya Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Korogwe vijijini kwa Karibu wa CCM Korogwe vijijini,Safina Alfred Nchinbi mkono wa kushoto leo katika ofisis za chama hicho.
 
 Picha ni Amina Magogo mara baada ya kuchukua fomu ya Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Korogwe vijijini akiionyesha kwa wasindikizaji nje mara baada ya kuchukua. 











Picha ni Amina Magogo mara baada ya kuchukua fomu ya Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Korogwe vijijini akiwa kwenye picha ya pamoja na wasindikizaji wake. 



Picha ni Amina Magogo mara baada ya kuchukua fomu ya Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Korogwe vijijini akieleza amejipanga kuwatumikia wananchi wa Korogwe vijijini nje ya ofisi za CCM baada ya kuchukua. 



Tuesday, 10 June 2025

MAPOKEZI YA MWENGW WA UHURU HALMASHAURI YA KOROGWE MJI 2025 ILIKUWA HIVI,

Picha Mkono wa kulia ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Kamishna William Mwakilema  akipokea Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa wilaya ya Handeni,Jafari Becha kushoto hafla iliyofanyika shule ya wasichana Korogwe Girls iliyopo wilayani hapo.

NA SOPHIA WAKATI,KOROGWE
MIRADI sita ya maendeleo ya wananchi iliyogharimu zaidi ya shilingi za kitanzania Billion moja,imekaguliwa,kufunguliwa na kuwekewa jiwe la msingi na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Mji Korogwe mkoani Tanga.

Akitoa taarifa kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa,Ismail Ally Usi,Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Kamishna William Mwakilema alisema katika miradi sita ipo itakayotembelewa,kuwekewa jiwe la msingi na kukaguliwa.

Awali Mkimbiza Mwenge Kitaifa,Ismail Ally Usi aliwataka wataalaam na watendaji kuhakikisha taarifa zote muhimu za miradi hiyo itakayotembelewa na Mwenge kuhakikisha zinakuwepo maeneo ya miradi sambamba na wataalam wahusika.

Kuhusu Mwenge wa Uhuru,Ismail alisema rais wa awamu ya kwanza Mwalimu Julias Nyerere aliamua upandishwe mlimani Kilimanjaro  kwa lengo la kumulika ukiangaza maeneo ya nchi ikiwa kiashiria cha kuimarisha Amani na kuleta na kuleta matumaini kwa Umma.

Alisema kwamba Halmashauri ya Mji Korogwe imetoa shilingi million 40 kwa ajili ya kuwawezesha vijana wa kikundi cha Bajaji na bodaboda ili kuweza kuimarisha shughuli zao za usafirishaji wilayani hapo.

Taarifa hiyo iliyotolewa na mmoja wa wanakikundi hao,akimweleza Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa,Ismail kuwa halimashauri yao imewawezesha ili kuweza kuboresha biashara yao ya usafirishaji na hivyo kuimarisha uchumi wao.

Msoma taarifa huyo alisema awali walianzisha kikundi chao hicho wakiwa na mtaji wa shilingi million 14 kabla ya serikal kupitia halmashauri kwa kutumia mapato ya ndani kuwapatia million 40hapo January 2022.

Alisema kuwa,baada ya kuwezeshwa fedha hizo na halmashauri waliongeza mtaji wao kwa kununua bajaji tatu huku wakiimarisha duka lao la vilainishi hatua ambayo imesaidia kukuza mtaji wao.

Akibainisha kuwa hivi sasa mtaji wao umekuwa na kuongezeka hadi kufikia shilingi million 54 za kitanzani huku wakifanikiwa kufanya marejesho kwa zaidi ya shilingi million sita.

Aidha,kupitia uimarishaji biashara yao hiyo vijana hao wa bodaboda na bajaji mbali na kujiajili kwa manufaa lakini pia wameweza kuajiri vijana wenzao ambao ni mafundi pikipiki.

Wameishukuru serikal kwa kuwapatia fedha hizo za mikopo ya asilimia kumi wakisema zimewasaidia kuongeza mtaji na kubadilisha maisha yao.
Mwisho.  

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa,Ismail mara baada ya kuwasili wilayani Korogwe akiwasalimia viongozi na watumishi mbalimbali wilayani hapo.



























Sunday, 2 March 2025

ZIARA YA RAIS DK.SAMIA SULUHU HASSAN YALETA MATUMAINI UPATIKANAJI WA MAJI SAFI NA SALAMA KWA WANANCHI MKINGA,,

Picha kulia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa Maji wa Mkinga – Horohoro uliopo katika Wilayani Mkinga, mkoani Tanga.

 NA SOPHIA WAKATI,MKINGA
SERIKAL kupitia Wizara ya Maji imekusudia kutekeleza mradi mkubwa wa Maji Mkinga – Horohoro, utakaotumia chanzo cha Bwawa la Mabayani kwa lengo la kumaliza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi katika maeneo ya mwambao wa Bahari ya Hindi mkoani Tanga.


Hayo yamethibitika kupitia mpango mkakati uliowekwa bayana kupitia ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye aliweka jiwe la msingi kwenye mradi huo wa Maji wa Mkinga – Horohoro uliopo katika Wilayani Mkinga, kwenye mkoa wa Tanga.


 Mradi huo unatarajiwa kugharamiwa na fedha za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania fedha kutoka Mfuko wa Taifa wa Maji ambapo kiasi cha Shilingi bilioni 35.47 zitatumika.


Katuka taarifa yake kwenye hafla hiyo, Waziri wa Maji, Jumaa Aweso alisema, wataalam wanaotekeleza mradi huo hawatasubiri mabomba yote yafike eneo la mradi 'site', isipokuwa wataendelea na kazi kwa kadiri mabomba yatakavyofika ili kukamilisha mradi kwa wakati.


Awali Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri alisema kuwa, mradi huo ulio chini ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkandarasi ni Kampuni ya STC Construction Ltd, ulianza novemba 5, 2022 unatarajiwa kukamilika 5 Oktoba, 2025.


Mhandisi Mwajuma alisema kuwa Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 35.47 kwa ajili ya mradi huo, huku tayari zaidi ya shilingi bilioni 11.32 zikiwa zimeshalipwa kwa mkandarasi anayehusika 


Alisema, kwa muda mrefu, wakazi wa vijiji 37 vilivyopo wilayani Mkinga wamekuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya maji wakitumia yake yenye chumvi, hali ambayo imechangia kuathiri shughuli za kila siku za uzalishaji.


Maji hayo wamekuwa wakitumia kwa matumizi ya nyumbani na kilimo na pindi mradi utakapokamilika  unatarajiwa kuboresha huduma ya maji safi na salama kwa wananchi zaidi ya 57,334 wa kata 10 katika vijiji 37 vilivyopo pembezoni mwa barabara ya Tanga - Horohoro pamoja na wananchi wa eneo la Horohoro lililopo Mpakani mwa Tanzania na Kenya.


Kukamilika kwa ujenzi wa mradi huo utakuwa ukombozi mkubwa kwa wananchi wa Mkinga ambao watakiwa wakipata maji safi na salama na hivyo kurahisisha utekelezaji wa majukumu mengine ya uzalishaji mali.
Mwisho.