Sunday 3 March 2024

UZINDUZI WA NYUMBA 23 KWA AJILI YA MAKAZI YA KUDUMU KWA WATOTO YATMA ILIKUWA HIVI 2024,,



Pichani katikati ni Meya wa halmashauri ya Jiji la Tanga, Abdarahman Shilloo akikata utepe hafla ya nyumba 23 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba.. 

NA SOPHIA WAKATI,TANGA
WATOTO Yatima 51 katika Halmashauri ya Jiji la Tanga wamenufaika na mradi wa Ujenzi Nyumba za makazi uliogharimu kiasi cha shilingi 652,000,000 Milioni hadi kukamilika.

 Meya wa Jiji la Tanga, Abdarahman Shilloo akikabidhi vyeti vya nyumba hizo 23 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba alisema ni jambo jema kwa jamii na serikal. 

Alisema Ujenzi wa nyumba hizo uliofanyika eneo la Bagamoyo mtaa wa Amani na Kilimani kata ya Tangasisi, ni matokeo ya ufadhili wa Waterfall Charity UK huku usimamizi ujenzi ukifanywa na taasisi ya Masjid Muzdalifa ya Jijini Tanga. 

Akizungumza baada ya kukabidhi hati za nyumba hizo kwa Yatima, Meya Shilloo amewapongeza Waterfall Charity UK kwa ufadhili na Masjid Muzdalifa kwa kusimamia kazi kwa uadilifu hadi kukamilika ujenzi wa makazi hayo.

"Bila Muzdalifa Waterfall isingefanya chochote. Imesimamia kazi kwa uadilifu na uangalifu mkubwa"alisema Shilloo huku akitanabaisha kuwa ni taasisi chache zenye uwezo kama ule wa Muzdalifa. 

Aidha amewataka Muzdalifa kuendelea na uaminifu wao hatua ambayo itawawezesha kuwa kiungo muhimu kati yao na jamii katika kuisaidia Serikali kwa maelezo kuwa majukumu yanayoikabili ni mengi hivyo inahitaji taasisi zenye kuzingatia uadilifu. 

Naye Katibu wa Masjid Muzdalifa,Twahir Twaha aliyemwakilisha Mkurugenzi wake Twaha Tawakal amewashukuru Waterfall Charity UK kwa ushirikiano waliouonesha hadi kufanikisha upatikanaji nyumba za watoto Yatima. 

Twaha alisema,uhitaji wa nyumba hizo ulionekana katika kipindi ambacho barabara ya Pangani Tanga ilikuwa ikipanuliwa kwa nyumba zilizopo jirani kubomolewa kupisha ujenzi.

"Mahitaji tuliyaona kupitia madarasani wanafunzi wetu wanaosoma walivyokuwa wakitaabika hapo tukagundua changamoto ya walezi kukosa makazi na tukawaomba Waterfall Charity UK kusaidia"alisema Twahir Twaha Tawakal. 

Twahir aliwaomba wadau wengine wakiwemo matajiri wenye fedha kujitokeza kusaidia watoto yatima na wale wanaoishi kwenye mazingira magumu ili nao kuweza kuishi Mama ilivyobkwa watoto wengine. 

Awali katika risala ya taasisi Mwalimu wa Shule ya Msingi ya mchepuo wa kiingereza Muzdalifa iliyopo Mwakidila, Ibadi Saidi alisema wamekuwa wakitoa elimu kwa Yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu. 

Aidha ameipongeza Waterfall Charity UK kukubali kulipia karo watoto yatima wanaosoma shule mbalimbali hususani sekondari akisema,taasisi hiyo tayari imetumia zaidi ya Shilingi 70.5 milioni. 

Kwa mujibu wa Mwalimu,Said aamesema azma waliyokuwa nayo kwa sasa ni kupata mfadhili ili kuweza kujenga shule ya sekobdari huku akimshukuru Serikali kwa kujipambanua katika kuhakikisha usalama kwa wageni na ameiomba kuangalia uwezekano kuweka unafuu wa kodi ya ardhi kwenye maeneo yanayokusudiwa kumilikishwa Yatima. 

Mwanamkasi Nuru ni mlezi wa mtoto Nuru Musa (14),baada ya kukabidhiwa hati ya kumiliki nyumba alisema,anaamini maisha yake na kijana wake yanakwenda kubadilika akiondoka kwenye mazingira duni yaliyokuwa yakimkabili.

Amewasilisha shukrani zake kwa asasi ya Waterfall Charity UK na Masjid Muzdalifa kwa ushirikiano waliouonesha hadi kuhakikisha Yatima wanapata nyumba watakazo tumia katika maisha yao. 
Mwisho.



Pichani ni Katibu wa Masjid Muzdalifa,Twahir Twaha aliyemwakilisha Mkurugenzi wake Twaha Tawakal akitumia nafasi hiyo kwa kuwashukuru Waterfall Charity UK kwa ushirikiano waliouonesha hadi kufanikisha upatikanaji nyumba za watoto Yatima. 









Pichani ni Miongoni mwa nyumba zilizojengwa.

 

Friday 2 February 2024

RC TANGA,KINDAMBA ATUMIA UFUNGUZI WA MAADHIMINI YA WIKI YA SHERIA 2024 KUWAASA WANAOSAMBAZA ABARI ZA UZUSHI KWENYE MITANDAO ,,

Pichani wa pili kutoka mkono wa kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba akiongoza matembezi ufunguzi maadhimisho ya Wiki ya sheria yaliyofanyika katika viwanja vya Tanga Urithi Jijini Tanga.

NA SOPHIA WAKATI,TANGA
MKUU wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba amesema,wanaoshiriki kusambaza habari za uzushi kwenye mitandao ya kijamii,hatua kali za kisheria hazitasita kuchukuliwa dhidi yao.

Kindamba aliyasema hayo alipokuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi maadhimisho ya Wiki ya sheria yanayofanyika katika viwanja vya Tanga Urithi Jijini Tanga.

Alielezea kusikitishwa kwake juu ya uzushi uliokuwa ukisambaa kupitia mitandao ya Kijamii kwamba mhanga mwingine wa ajali iliyohusisha msafara wa Naibu Waziri Mkuu Dk. Doto Biteko kudaiwa kufariki dunia.

Alisema, mhanga huyo amekuwa akiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa Bombo na.kwamba ameanza kupata utambuzi licha ya awali kuwa katika hali mbaya.

"Hakuna faida yeyote kumsingizia mtu kifo sote njia ni hiyo hiyo hata uwe na fedha cheo iko siku na wewe utakwenda, jambo lililotendeka kwenye mitandao sikulipenda na kilichofanyika ni kosa la jinai"alisema Mkuu huyo wa mkoa Kindamba.

Kutokana na hali hiyo Kindamba alisema kwamba,hatua za kisheria zitachukuliwa kwa aliyeanzisha,aliyesambaza na hata kulikoleza jambo hilo ovu kwenye mitandao ya kijamii.

"Kiukweli tutawasaka na tutawachukulia hatua kali na hili ni kosa la mtandao,haina sababu kusingizia mwenzako kifo"alisema Kindamba kwa masikitiko makubwa. 

''Hivi majuzi Naibu Waziri Mkuu Dk. Doto Biteko aliyekuwa ziarani Mkoani Tanga gari walilopanda baadhi ya Waandishi wa habari na watumishi wa Tanga Uwasa waliokuwa kwenye msafara wake lilipata ajali''Alisema.

Ajali hiyo ilisababisha majeruhi ambao waliwahishwa Hospitali ya Bombo kwa ajili ya kupata matibabu ingawa kwa bahati mbaya mwandishi wa kituo cha Tanga TV Ally Haruna na Saidi Alawi dereva wa gari la Tanga Uwasa walifariki.

Haruna alizikwa kwenye makaburi ya Sharif Haidar Msamweni Jijini Tanga na Alawi alizikwa wilayani Pangani iliyopo mkoani Tanga ambapo kwenye ufunguzi Maadhimisho hayo Wiki ya sheria  Mahakama kuu kanda ya Tanga,Kindamba alitumia nafasi hiyo kwa kuwataka wadau kutumia muda mfupi kusimama kuwaombea Marehemu na wahanga wa ajali hiyo wapate kupona haraka kurejea kwenye majukumu yao.

Hata hivyo alisema serikali itaendelea kuwa nao bega kwa bega katika kuhakikisha wahanga wanapatiwa huduma stahiki ili atya zao kuweza kuimarika.
Mwisho.















 

Monday 29 January 2024

WANANCHI WILAYANI MUHEZA WANATARAJIWA KUNUFAIKA NA FEDHA ZA TOZO YA MAFUTA KUKARABATI BARABARA ZINAZOTUMIKA KWENYE MASHAMBA YA MACHUNGWA,,,



Pichani ni Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini TARURA Wilayani Muheza, Mhandisi John Frank Kwagilwa akiwa miongoni mwa barabara zilizopata fedha ya utekelezaji miradi kutoka serikalini.

NA SOPHIA WAKATI,MUHEZA
WANANCHI wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga wanatarajia kunufaika na fedha za tozo ya mafuta baada ya kupata Milioni 950,220,000 ambazo zitatumika katika kufanya matengenezo kwenye miundombinu ya barabara zao.

 Taarifa hiyo imetolewa na Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini TARURA Wilayani Muheza,Mhandisi John Frank Kwagilwa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Wilayani humo.

Alisema kwamba kupitia fedha hizo barabara nyingi zitafanyiwa kazi zikiwemo zile zitakazounganisha vijiji vyenye Wakulima wa matunda hatua ambayo huenda ikasaidia kuleta tija kwenye sekta ya kilimo.

''Kuna fedha kutoka mfuko wa tozo kutoka Serikalini Shilingi 950,220,000 Milioni zitatumika kujenga barabara nyingi kwa kiwango cha changarawe''alisema Mhandisi huyo wa TARURA Muheza Kwagilwa.

AidA,Amezitaja barabara hizo zitakazofanyiwa matengenezo kuwa niza vijiji vya Kwakopwe - Mapinduzi 2.4 Km, Makuyuni - Kimwagamchuzi 2.8 Km, Makuyuni - Buhuri 4Km na Kwafungo - Kilongo 3.5 Kilomita na pia kunatarajiwa kujengwa vivuko.

Pia kuna barabara za Misozwe - Kwetango - Kambai - Msige 5 Km ,Mdote - Tanesco 0.6 Km, Genge - Mang'enya 2.0 Km, Muheza High school - Kivindo 1.66, Muheza Estate - Mkumbi 2.0 Km, Shidepha - Kididima 1.17 Km na Kwemuyu TRM - Ofisi ya Kata/Barabara ya Majengo 1.17.

Matengenezo mengine ni Box culvert,pipe culvert na matengenezo ya kawaida Mikwamba-Magila-Magoroto 4.0 Km, Amani-Kibaoni - Derema - Bulwa - Zirai -Bebere 5.0 Km,Mgeza - Kiwandamwenyeji 2.0 Km.

Kwa mujibu wa Mhandisi Kwagilwa alibainisha kwamba ujenzi wa barabara hizo ni matokeo ya kupokea mapendekezo kutoka kwenye vikao vya Kata ambavyo wenyeviti wake ni madiwani wanaopokea maoni ya Wananchi wialayani hapo.

 Katika utekelezaji huo wa mradi,Mhandisi Kwagilwa alisema kuwa, wananchi watapewa kipaumbele kwenye ajira za muda mara baada ya wakandarasi kutambulishwa lengo likiwa kuimarishwa kwa mahusiano ili kuleta ufanisi pindi mradi utakapokuwa ukitekelezwa.

Ujenzi wa mradi huo unatarajiwa kuanza mara baada ya michakato kukamilika hatua inayoendelea ni mchakato wa manunuzi na kuchukua nafasi yake na kazi tayari zimeshatangazwa.
Mwisho. 




 

Picha zote ni Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini TARURA Wilayani Muheza, Mhandisi John Frank Kwagilwa akiwa miongoni mwa barabara zilizopata fedha ya utekelezaji miradi kutoka serikalini.

WAFANYAKAZI WA SHIRIKA LA UMEME ZANZIBAR ZECO WAWEKA HISTORIA YA KUTEMBELEA VITUO VYA KUZALISHA UMEME 2024 TANGA,,



BAADA ya kutembelea Vituo vya Pangani  Hydro  Syestem Wafanyakazi wa Shirika la nishati ua Umeme Visiwani Zanzibar wamesema,ushirikiano na wenzao wa Tanesco utaimarika na hivyo kumudu kutatua mambo mengi kwa muda mfupi. 


Mkuu wa udhibiti mapato wa Shirika la Umeme Zanzibar Electricity Corporation (ZEC), Faina Idarus Faina amesema,katika ziara yao ya mafunzo mwaka 2024 tija itaonekana kwa Wafanyakazi wa pande zote mbili za Muungano.

Alisema,licha ya wao kushughulika na suala la Nishati hiyo ya Umeme kwa kuwahudumia Wananchi wa Visiwa vya Zanzibar lakini walikosa kujua namna ambavyo Nishati hiyo muhimu imekuwa ikizalilshwa.

Faina aliendelea kusema kwamba, ziara hiyo imekuwa darasa muhimu kwao, kwani waweza kujifunza mambo wasiyoyajua huku wakiimarisha uhusiano na wafanyakazi wenzao wa Tanzania bara.

Alisema,elimu waliyopata itawasaidia katika kuwaelimisha wateja wanaowahudumia pindi wanapolalamikia mambo ambayo hayakutokea kwa makusudi ila ni changamoto za kitaalam.

"Tumejua mengi ambayo hatukuwahi kuyajua,sie tumekuwa tukinunua umeme Tanzania bara kwa bulk na tunauza kwa wananchi"alisema Faina na kuongeza.

"Ziara yetu tumejifunza mengi,tumeimarisha uhusiano sasa tutatatua mambo mengi kwa wakati mmoja...pia tumepata elimu tutawaelimisha wateja wetu pindi wanapopiga yowe kukatika kwa umeme maana huwa sio kusudi"alisema Faina. 

Naye Kaimu Meneja wa Vituo vya kuzalisha Nishati ya Umeme Pangani Hydro Syestem, Kulwa Sosthenes alisema, wafanyakazi hao wa ZECO wametembelea vituo vya kuzalisha umeme wa nguvu ya maji New Pangani Force.

Sosthenes alisema kwamba,wageni hao wamejifunza jinsi umeme unavyozalishwa huku wakifahamiana na wenzao wa Tanzania bara hatua ambayo anaamini itaimarisha mahusiano na pia kuleta tija maeneo ya kazi.

Katika siku ya kwanza ya ziara yao Jijini Tanga,wakiwa wameambatana na Mbunge wa Jimbo la Amani Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar, Abdul Yusuph Maalim, aliishauri Serikali kutenga fedha kwa ajili ya ziara za mafunzo kwa wafanyakazi wa taasisi. 

Mwisho. 



 Pichani ni mkuu wa kituo cha Hale Pangani  Hydro  Syestem,Kulwa Sosthenes akiwa ofisini kwake mara baada ya kuwapokea wafanyakazi wa shirika la umeme  ZECO Zanzibar.



Pichani ni kocha wa timu ya Soka ya Tanesco Tanga,Chausa Mganga akitangaza kuifua kikosi chake.

Kocha wa timu ya Soka ya Tanesco Tanga,Chausa Mganga ameahidi kuongeza makali mwaka 2024 kwenye kikosi chake hatua ambayo itawawezesha kupata ushindi mnono dhidi ya wapinzaji wake ambao watashuka dimbani kucheza michezo mbali mbali ikiwemo na ZECO kutoka Visiwani Zanzibar.


Chausa ametoa Matambo hayo Jiiini Tanga mara baada ya michezo ya Kirafiki dhidi ya Tanesco ya Zanzibar na matokeo ya mtanange huo uliopigwa Viwanja vya Popatlal yalikuwa mabao 2-2.

Baada ya michezo hiyo uliokuwa na upinzani mkali uliofanikiwa kuteka mashabiki wengi kutoka ndani ya Jiji la Tanga Viongozi wa timu zote mbili waliowapa fursa ya kutoa maoni yao.

Meneja wa Shirika la Umeme Tanesco Mkoani Tanga,Mathias Solongo aliyekuwepo kwenye mchezo huo alisema,licha ya kukubaliana na matokeo ya mchezo huo.lakini anaamini Vijana wake wangeweza kupata matokeo mazuri zaidi.

Alisema,vijana wake chini ya Mwalimu wao Chausa Mganga walionesha mchezo mzuri ikiwa ni ishara kwamba wameyaelewa mafunzo waliyopew na Mwalimu wao.

Hata hivyo,alisema kuwa pengine kilichowasababisha kupata sare hiyo ni kasoro ndogo ndogo ambazo sasa zitakwenda kufanyiwa kazi na kuwawezesha kupata ushindi kwa kila mchezo.

Ili waweze kufanya vyema kwenye michezo yao, Mhandisi Solongo alisema atahakikisha vijana hao wanapata maandalizi maazuri yatakayowawezesha kupata ushindi mchezoni.

"Timu yangu ni nzuri na niseme tu tutaendelea na.maandalizi ya kujiwinda kwa mchezo wa marudiano,nasi tutatafuta nafasi ya kuwafuata kule Zanzibar"alisema Solongo huku akiahidi kwenda kipata ushindi.

Naye Kiongozi wa timu ya Shirika la umeme Zanzibar Electricity Corporation (ZECO), alisema kwamba,hakuna ushindi wa kirahisi utakaopatikana kutoka kwa Vijana wake.

Alijinadi kuwa timu yake ni bora na Tanesco Tanga wajiandae kupogea kipigo pindi watakapokanyaga ardhi ya Visiwa vya Zanzibar. 

Pamoja na hayo pia alielezea kuridhishwa kwake na mapokezi mazuri waliyopata kutoka kwa wenyeji wa Tanesco Tanga akisema wamefarijika kwa ujarimu na ushirikiano waliopata.

Alisema kuwa,ziara hiyo ya michezo imewawezesha kujifunza mambo mbalimbali hatua ambayo itasaidia kuongeza ufanisi kwenye majukumu yao ya kazi. 

Mwisho.

 

Monday 1 January 2024

WANANCHI ZAID YA 600,000 WANATARAJIWA KUNUFAIKA NA MRADI MKUBWA WA MAJI MIJI 28,

Pichani ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira, Handeni Trunk Main (HTM),Mhandisi Yohana Mgaza akizungumza na waandishi wa habari  Ofisini kwake juu ya utekelezaji wa mradi mkubwa na wananchi wanaotarajiwa kunufaika..

NA SOPHIA WAKATI,KOROGWE

ZAIDI ya Watu 600,000 wanatarajiwa kunufaika na upatikanaji wa huduma ya Maji Safi na salama kupitia utekelezwaji Ujenzi Mradi mkubwa wa Maji wa Miji 28 ambao utazigusa Wilaya za Korogwe, Handeni, Muheza na Pangani zilizopo katika Mkoa wa Tanga.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira, Handeni Trunk Main (HTM), Yohana Mgaza alitoa taarifa wakaTi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake.

Mgaza ambaye kitaaluma ni Mhandisi alisema, utekelezwaji mradi huo tayari umeshaanza ambapo chanzo cha Maji hayo itakuwa Mto Pangani kutoka kwenye Kijiji cha Mswaha Darajani wilayani Korogwe.

Mradi huo unatekelezwa na Kampuni ya M/s Jwil Infra Construction Limited na Kampuni Mshauri ni WAPCOS zote za nchini India ambapo wasimamizi Handeni Trunk Main kwa niaba ya Wizaya ya Maji.

Mhandisi Mgaza alisema kuwa fedha nyingi za Serikali zitatumika kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji Mradi huo lengo likiwa kutimiza azma ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kumtua Mama ndoo kichwani.

Mgaza alisema kwamba, kwa wilaya hizo nne (4) za Pangani, Muheza, Korogwe na Handeni Mradi utagharimu Shiulingi Bilioni 200 ambapo Wataalam wa HTM watahakikisha unajengwa kwa viwango stahiki.

Akizungumzia zaidi shughuli za ujenzi wa mradi huo, Mgaza alisema kule kwenye chanzo ambapo ni eneo la Kijiji cha Mswaha Darajani kutajengwa Mtambo wa kuchuja Maji kabla ya kuanza kusambazwa.

Vilevile alisema kwamba,kazi kadhaa zimeendelea kufanyika akitaja ujenzi wa matenki ya kuhifadhia Maji huku mengine yakiwa kwenye hatua ya kuwekwa Zege ili kuyawezesha kuhifadhio Maji ya kutosha.

Pamoja na hayo Mgaza aliishukuru Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassani kwa kuwezesha upatikanaji wa fedha ambazo leo zinawezesha utekelezwaji mradi huo mkubwa wa Maji.

Aidha Mgaza alisema ujenzi mradi wa Maji kwa Miji minne Mkoani Tanga utaongeza kipato cha Wananchi kwa vile Vijana watahitajika kwenye ujenzi huku akina Mama wakishiriki kupika na kuuza chakula.

Mwisho.


 

Monday 25 December 2023

TANESCO TANGA NA ZECO ZANZIBAR ZATOKA SARE YA 2-2,PAMBANO LA KIRAFIKI ZIARA YAO MKOANI TANGA 2023.



Pichani mkono wa kushoto ambaye amesimama ni Meneja wa Tanesco Mkoani Tanga Mathias Solongo akizungumza na wachezaji wa Tanesco Tanga na Zeco ya Zanzibar akieleza kuridhishwa kwake na mchezo huo wa kirafiki kuimarisha mahusiano kazini na kujenga urafiki.
NA SOPHIA WAKATI,TANGA
TIMU za Soka Tanesco Tanga na ile ya Shirika la kuzalisha Nishati ya Umeme ZECO Zanzibar zimeshindwa kutambia  baada ya kutoka Sare ya magoli 2 - 2.

Katika mchezo huo wa vuta nikuvute uliopigwa Jana viwanja vya Popatlal Jijini Tanga, timu ya Zeco ..ndio ilikuwa ya kwanza kuliona lango la wapinzani wao.

Zeco Zanzibar ilianza kuandika goli lake dakika 21 kipindi Cha kwanza kupitiaNabil Hamoor juma Jaja ambalo liliongeza nguvu ya mashambulizi katik mchezo huoAlly Salim.

Baada ya kuongia Kwa goli Hilo,Tanesco Tanga ilijipanga na kusawadhisha kupitia Jackson Chilu dakika 31 na Faidin Kombo dakika ya 47 ambayo yalikuwa muhimu katika mchezo huo.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ya aina yake kila timu kuongezea mashambulizi ambap Kwa Zeco yalileta mafanikio baada ya mchezaji Seleman Rashid dakika ya 65 kuifungia goli la pili ambalo liliwapa nguvu kuondoka uwanjani hapo huku goli la pili likifungwa na  Ally Salim ambalo lilikuwa muhimu katika mchezo huo.

Kocha wa timu ya Zeco  Zanzibar,Seifu Mzee Aweso alisema,mchezo huo ulikuwa mzuri ingawa awali wapinzani wao walionekana kumudu kuutawa mchezo huo,lengo ni kufanya ziara na kubadilisha mawazo na kujenga uzoefu sehemu ya kazi.

Katibu msaidizi wa timu Zeco,Mgaza Mhaya Ramadhan amesema amekuja na timu ya watu 53 wakiwemo wachezaji na viongozi kufanya ziara ya siku nne ikiwemo kucheza mechi za kirafiki na wenyeji wao Tanesco ya mkoa wa Tanga.

Alisema,hali ilitokana na wao ZECO kukosa muda wa kufanya mazoezi ya maandalizi tangu walipoingia Jijini Tanga ingawa mapungufu yaliyoonekana mchezoni walimu waliyafanyia kazi.

Meneja wa Tanesco Mkoani Tanga Mathias Solongo alielezea kuridhishwa kwake na mchezo huo wa kuimarisha mahusiano akisema umechezwa kwa nidhamu ya hali ya juu kwa vipindi vyote.

"Nitaendelea kuimarisha kikosi changu,kuwapa muda wachezaji kufanya mazoezi kujiandaa na mashindano yoyote ambayo yayajitokeza"Alisema Meneja huyo Solongo.
Mwisho.

NA SOPHIA WAKATI,TANGA
MBUNGE wa Chama Cha Mapinduzi CCM Jimbo la Amani Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar, Abdul Yusuph Maalim ameshauri kuwekwa Ligi fupi ya Soka itakayohusiana na mambo ya Muungano. 

Ushauri huo umetolewa jana Viwanja vya Popatlal Jiiini Tanga, katika ziata ya siku MBUNGE huyo Maalim alisema kwamba uwepo wa Ligi hiyo utasaidia katika kuimarisha Muungano uliopo nchini. 

Alisema kwamba,ligi hiyo itakayokuwa ya Muungano ni vyema ikazihusisha timu za taasisi za Serikali akitolea mfano wa Tanesco,ZECO ya Zanzibar hatua aliyoieleza kuwezesha undugu kuimarika.

"Iwekwe ligi fupi ya Mashirika  itakayohusiana na mambo ya Muungano Tanesco, Zeco Zanzibar na wengine kuzidi kujenga udugu tuliokuwa nao na Muungano wetu"alisema Maalim. 

Pamoja na hayo Maalim alisema,iko haja kwa Serikali kuyenga bajeti ndogo kwa ajili ya Wafanyakazi kufanya ziara za mafunzo na hata michezo inayowasaidia kujenga mahusiano. 

Alisema,anafamu kiwa Serikali ina mzigo mzito ila ziara hizo za mafunzo kwa wafanyakazi nazo zina umuhimu katika kuongeza tija kazini. 

"Ifike muda kuwe na bajeti maalum kwenye hizi taasisi,tunajua Serikali ina mzigo mzito ila bajeti ndogo italeta tija baada ya mfanyakazi kuwa kazini muda mrefu"alisema Maalim. 

Mbunge Maalim kabla ya kutumbukia kwenye Siasa alipata kuwa mfanyakazi wa ZECO Zanzibar ambapo amesema taasisi nyingi za Serikali zinafanya Safari kwa kuiitegemea.

Katika mchezo huo wa Kirafiki kati ya ZECO Zanzibar na Tanesco Tanga matokeo yalikuwa mabao 2 kwa 2 huku mchezo ukiwa wenye upinzani mkali. 

Akizungumzia mchezo huo Meneja wa Tanesco Mkoani Tanga Mathias Amon Solongo alisema,ulikuwa wenye kuvutia na ulichezwa kimsingi wa ustaarabu.

Aliwashukuru wanamichezo walioshiriki mchezo huo huku akiahidi kukipeleka Zanzibar kikosi cha timu ya Tanesco ya Tanga.

Mwisho







 

Monday 4 December 2023

POLISI TANGA YASHIKILIA BOTI KWA KUTUMIKA KWA UVUVI HARAMU WA KUTUMIA BARUTI,,,



Pichani ni Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga,Almachius Mchunguzi akieleza jinsi polisi walivyofanikiwa kukamata boti iliyokuwa inatumika kwa uvuvi haramu.

NA SOPHIA WAKATI,TANGA
JESHI la polisi mkoani Tanga linashikilia Boti aina ya Fible ambayo inadaiwa kutumiwa na Wavuvi kwa kuvua Samaki kinyume na taratibu za kisheria kwa kutumia 'Baruti',.

Kamanda wa jeshi la polisi Mkoani Tanga,Almachius Mchunguzi akithibitisha kutokea kwa tukio hilo alisema polisi wakiwa doria za majini na kuitilia shaka boti hiyo na kuifuatilia wavuvi walikimbia kusiko julikana.

Alisema kwamba tukio hilo lilitokea Novemba 21/11/2023 huko bahari ya Hindi katika Kisiwa cha Jambe kilichopo Wilayani Tanga huku ikiwa na kilogram 30 za samaki.

"Polisi tunashikilia boti ya uvuvi na samaki kilogram 30,baada ya kuikama tunafuatili kuwasaka wahusika,taratibu nyingine ziweze kuchukuliwa dhidi yao''Alisema kamanda Mchunguzi.

Alisema kuwa, katika Operesheni zake, Polisi wamefanikiwa kukamata boti moja aina ya Fible ambayo ilikuwa na Wavuvi wanaotumia baruti pindi wanapovua Samaki.

Aidha alisema kwamba, wavuvi hao walifanikiwa kukimbia huku boti iliyokuwa na Kilogramu 30 za Samaki wa aina mbalimbali waliitelekeza ikishikiliwa na Jeshi la Polisi.

"Polisi tumejipanga kuimarisha doria kufanya nchi kavu na Baharini, ambapo sasa hivi zimeanza kuzaa matunda tarehe 21 Novemba katika Kisiwa cha Jambe Wilayani Tanga Polisi tumefanikiwa kukamata boti aina ya 'Fible' ikiwa na wavuvi wanaotumia baruti"alisema Mchunguzi. 

Hata hivyo,Kamanda Mchunguzi alisema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea ili hatua kuchukuliwa kwa wale watakaobainika kuhusika na suala hilo ambalo ni kinyume na taratibu za sheria.

Katika tukio jingine, Kamanda Mchunguzi alisema, watu 21 wamekamatwa na bangi Kg 43, Mirungi Kg 124.5 na Heroine gram 242 huku watuhumiwa wanne wakikamatwa kwa kusafirisha wahamiaji haramu.

Vilevile watuhumiwa saba (7) ambao ni raia wa Ethiopia wamekamatwa kwa kuingia nchini pasipokuwa na vibali.

Pamoja na hayo tukio jingine linamuusisha mtu mmoja aliyekamatwa kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia Silaha aliyoitaja kuwa ni Panga.

Kamanda Mchunguzi alisema kuwa ni moja sehemu ya mafanikio ya Jeshi la Polisi ambapo katika kipindi cha mwezi mmoja yaani Oktoba 22 mpaka Nov 27,2023 ambapo pia Polisi walikamata watu 107 katika misako mbalimbali Mkoani Tanga. 
Mwisho.