Sunday 3 March 2024

UZINDUZI WA NYUMBA 23 KWA AJILI YA MAKAZI YA KUDUMU KWA WATOTO YATMA ILIKUWA HIVI 2024,,



Pichani katikati ni Meya wa halmashauri ya Jiji la Tanga, Abdarahman Shilloo akikata utepe hafla ya nyumba 23 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba.. 

NA SOPHIA WAKATI,TANGA
WATOTO Yatima 51 katika Halmashauri ya Jiji la Tanga wamenufaika na mradi wa Ujenzi Nyumba za makazi uliogharimu kiasi cha shilingi 652,000,000 Milioni hadi kukamilika.

 Meya wa Jiji la Tanga, Abdarahman Shilloo akikabidhi vyeti vya nyumba hizo 23 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba alisema ni jambo jema kwa jamii na serikal. 

Alisema Ujenzi wa nyumba hizo uliofanyika eneo la Bagamoyo mtaa wa Amani na Kilimani kata ya Tangasisi, ni matokeo ya ufadhili wa Waterfall Charity UK huku usimamizi ujenzi ukifanywa na taasisi ya Masjid Muzdalifa ya Jijini Tanga. 

Akizungumza baada ya kukabidhi hati za nyumba hizo kwa Yatima, Meya Shilloo amewapongeza Waterfall Charity UK kwa ufadhili na Masjid Muzdalifa kwa kusimamia kazi kwa uadilifu hadi kukamilika ujenzi wa makazi hayo.

"Bila Muzdalifa Waterfall isingefanya chochote. Imesimamia kazi kwa uadilifu na uangalifu mkubwa"alisema Shilloo huku akitanabaisha kuwa ni taasisi chache zenye uwezo kama ule wa Muzdalifa. 

Aidha amewataka Muzdalifa kuendelea na uaminifu wao hatua ambayo itawawezesha kuwa kiungo muhimu kati yao na jamii katika kuisaidia Serikali kwa maelezo kuwa majukumu yanayoikabili ni mengi hivyo inahitaji taasisi zenye kuzingatia uadilifu. 

Naye Katibu wa Masjid Muzdalifa,Twahir Twaha aliyemwakilisha Mkurugenzi wake Twaha Tawakal amewashukuru Waterfall Charity UK kwa ushirikiano waliouonesha hadi kufanikisha upatikanaji nyumba za watoto Yatima. 

Twaha alisema,uhitaji wa nyumba hizo ulionekana katika kipindi ambacho barabara ya Pangani Tanga ilikuwa ikipanuliwa kwa nyumba zilizopo jirani kubomolewa kupisha ujenzi.

"Mahitaji tuliyaona kupitia madarasani wanafunzi wetu wanaosoma walivyokuwa wakitaabika hapo tukagundua changamoto ya walezi kukosa makazi na tukawaomba Waterfall Charity UK kusaidia"alisema Twahir Twaha Tawakal. 

Twahir aliwaomba wadau wengine wakiwemo matajiri wenye fedha kujitokeza kusaidia watoto yatima na wale wanaoishi kwenye mazingira magumu ili nao kuweza kuishi Mama ilivyobkwa watoto wengine. 

Awali katika risala ya taasisi Mwalimu wa Shule ya Msingi ya mchepuo wa kiingereza Muzdalifa iliyopo Mwakidila, Ibadi Saidi alisema wamekuwa wakitoa elimu kwa Yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu. 

Aidha ameipongeza Waterfall Charity UK kukubali kulipia karo watoto yatima wanaosoma shule mbalimbali hususani sekondari akisema,taasisi hiyo tayari imetumia zaidi ya Shilingi 70.5 milioni. 

Kwa mujibu wa Mwalimu,Said aamesema azma waliyokuwa nayo kwa sasa ni kupata mfadhili ili kuweza kujenga shule ya sekobdari huku akimshukuru Serikali kwa kujipambanua katika kuhakikisha usalama kwa wageni na ameiomba kuangalia uwezekano kuweka unafuu wa kodi ya ardhi kwenye maeneo yanayokusudiwa kumilikishwa Yatima. 

Mwanamkasi Nuru ni mlezi wa mtoto Nuru Musa (14),baada ya kukabidhiwa hati ya kumiliki nyumba alisema,anaamini maisha yake na kijana wake yanakwenda kubadilika akiondoka kwenye mazingira duni yaliyokuwa yakimkabili.

Amewasilisha shukrani zake kwa asasi ya Waterfall Charity UK na Masjid Muzdalifa kwa ushirikiano waliouonesha hadi kuhakikisha Yatima wanapata nyumba watakazo tumia katika maisha yao. 
Mwisho.



Pichani ni Katibu wa Masjid Muzdalifa,Twahir Twaha aliyemwakilisha Mkurugenzi wake Twaha Tawakal akitumia nafasi hiyo kwa kuwashukuru Waterfall Charity UK kwa ushirikiano waliouonesha hadi kufanikisha upatikanaji nyumba za watoto Yatima. 









Pichani ni Miongoni mwa nyumba zilizojengwa.

 

No comments:

Post a Comment