Friday 2 February 2024

RC TANGA,KINDAMBA ATUMIA UFUNGUZI WA MAADHIMINI YA WIKI YA SHERIA 2024 KUWAASA WANAOSAMBAZA ABARI ZA UZUSHI KWENYE MITANDAO ,,

Pichani wa pili kutoka mkono wa kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba akiongoza matembezi ufunguzi maadhimisho ya Wiki ya sheria yaliyofanyika katika viwanja vya Tanga Urithi Jijini Tanga.

NA SOPHIA WAKATI,TANGA
MKUU wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba amesema,wanaoshiriki kusambaza habari za uzushi kwenye mitandao ya kijamii,hatua kali za kisheria hazitasita kuchukuliwa dhidi yao.

Kindamba aliyasema hayo alipokuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi maadhimisho ya Wiki ya sheria yanayofanyika katika viwanja vya Tanga Urithi Jijini Tanga.

Alielezea kusikitishwa kwake juu ya uzushi uliokuwa ukisambaa kupitia mitandao ya Kijamii kwamba mhanga mwingine wa ajali iliyohusisha msafara wa Naibu Waziri Mkuu Dk. Doto Biteko kudaiwa kufariki dunia.

Alisema, mhanga huyo amekuwa akiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa Bombo na.kwamba ameanza kupata utambuzi licha ya awali kuwa katika hali mbaya.

"Hakuna faida yeyote kumsingizia mtu kifo sote njia ni hiyo hiyo hata uwe na fedha cheo iko siku na wewe utakwenda, jambo lililotendeka kwenye mitandao sikulipenda na kilichofanyika ni kosa la jinai"alisema Mkuu huyo wa mkoa Kindamba.

Kutokana na hali hiyo Kindamba alisema kwamba,hatua za kisheria zitachukuliwa kwa aliyeanzisha,aliyesambaza na hata kulikoleza jambo hilo ovu kwenye mitandao ya kijamii.

"Kiukweli tutawasaka na tutawachukulia hatua kali na hili ni kosa la mtandao,haina sababu kusingizia mwenzako kifo"alisema Kindamba kwa masikitiko makubwa. 

''Hivi majuzi Naibu Waziri Mkuu Dk. Doto Biteko aliyekuwa ziarani Mkoani Tanga gari walilopanda baadhi ya Waandishi wa habari na watumishi wa Tanga Uwasa waliokuwa kwenye msafara wake lilipata ajali''Alisema.

Ajali hiyo ilisababisha majeruhi ambao waliwahishwa Hospitali ya Bombo kwa ajili ya kupata matibabu ingawa kwa bahati mbaya mwandishi wa kituo cha Tanga TV Ally Haruna na Saidi Alawi dereva wa gari la Tanga Uwasa walifariki.

Haruna alizikwa kwenye makaburi ya Sharif Haidar Msamweni Jijini Tanga na Alawi alizikwa wilayani Pangani iliyopo mkoani Tanga ambapo kwenye ufunguzi Maadhimisho hayo Wiki ya sheria  Mahakama kuu kanda ya Tanga,Kindamba alitumia nafasi hiyo kwa kuwataka wadau kutumia muda mfupi kusimama kuwaombea Marehemu na wahanga wa ajali hiyo wapate kupona haraka kurejea kwenye majukumu yao.

Hata hivyo alisema serikali itaendelea kuwa nao bega kwa bega katika kuhakikisha wahanga wanapatiwa huduma stahiki ili atya zao kuweza kuimarika.
Mwisho.















 

No comments:

Post a Comment