Monday 29 January 2024

WANANCHI WILAYANI MUHEZA WANATARAJIWA KUNUFAIKA NA FEDHA ZA TOZO YA MAFUTA KUKARABATI BARABARA ZINAZOTUMIKA KWENYE MASHAMBA YA MACHUNGWA,,,



Pichani ni Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini TARURA Wilayani Muheza, Mhandisi John Frank Kwagilwa akiwa miongoni mwa barabara zilizopata fedha ya utekelezaji miradi kutoka serikalini.

NA SOPHIA WAKATI,MUHEZA
WANANCHI wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga wanatarajia kunufaika na fedha za tozo ya mafuta baada ya kupata Milioni 950,220,000 ambazo zitatumika katika kufanya matengenezo kwenye miundombinu ya barabara zao.

 Taarifa hiyo imetolewa na Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini TARURA Wilayani Muheza,Mhandisi John Frank Kwagilwa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Wilayani humo.

Alisema kwamba kupitia fedha hizo barabara nyingi zitafanyiwa kazi zikiwemo zile zitakazounganisha vijiji vyenye Wakulima wa matunda hatua ambayo huenda ikasaidia kuleta tija kwenye sekta ya kilimo.

''Kuna fedha kutoka mfuko wa tozo kutoka Serikalini Shilingi 950,220,000 Milioni zitatumika kujenga barabara nyingi kwa kiwango cha changarawe''alisema Mhandisi huyo wa TARURA Muheza Kwagilwa.

AidA,Amezitaja barabara hizo zitakazofanyiwa matengenezo kuwa niza vijiji vya Kwakopwe - Mapinduzi 2.4 Km, Makuyuni - Kimwagamchuzi 2.8 Km, Makuyuni - Buhuri 4Km na Kwafungo - Kilongo 3.5 Kilomita na pia kunatarajiwa kujengwa vivuko.

Pia kuna barabara za Misozwe - Kwetango - Kambai - Msige 5 Km ,Mdote - Tanesco 0.6 Km, Genge - Mang'enya 2.0 Km, Muheza High school - Kivindo 1.66, Muheza Estate - Mkumbi 2.0 Km, Shidepha - Kididima 1.17 Km na Kwemuyu TRM - Ofisi ya Kata/Barabara ya Majengo 1.17.

Matengenezo mengine ni Box culvert,pipe culvert na matengenezo ya kawaida Mikwamba-Magila-Magoroto 4.0 Km, Amani-Kibaoni - Derema - Bulwa - Zirai -Bebere 5.0 Km,Mgeza - Kiwandamwenyeji 2.0 Km.

Kwa mujibu wa Mhandisi Kwagilwa alibainisha kwamba ujenzi wa barabara hizo ni matokeo ya kupokea mapendekezo kutoka kwenye vikao vya Kata ambavyo wenyeviti wake ni madiwani wanaopokea maoni ya Wananchi wialayani hapo.

 Katika utekelezaji huo wa mradi,Mhandisi Kwagilwa alisema kuwa, wananchi watapewa kipaumbele kwenye ajira za muda mara baada ya wakandarasi kutambulishwa lengo likiwa kuimarishwa kwa mahusiano ili kuleta ufanisi pindi mradi utakapokuwa ukitekelezwa.

Ujenzi wa mradi huo unatarajiwa kuanza mara baada ya michakato kukamilika hatua inayoendelea ni mchakato wa manunuzi na kuchukua nafasi yake na kazi tayari zimeshatangazwa.
Mwisho. 




 

Picha zote ni Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini TARURA Wilayani Muheza, Mhandisi John Frank Kwagilwa akiwa miongoni mwa barabara zilizopata fedha ya utekelezaji miradi kutoka serikalini.

No comments:

Post a Comment