Monday 29 January 2024

WAFANYAKAZI WA SHIRIKA LA UMEME ZANZIBAR ZECO WAWEKA HISTORIA YA KUTEMBELEA VITUO VYA KUZALISHA UMEME 2024 TANGA,,



BAADA ya kutembelea Vituo vya Pangani  Hydro  Syestem Wafanyakazi wa Shirika la nishati ua Umeme Visiwani Zanzibar wamesema,ushirikiano na wenzao wa Tanesco utaimarika na hivyo kumudu kutatua mambo mengi kwa muda mfupi. 


Mkuu wa udhibiti mapato wa Shirika la Umeme Zanzibar Electricity Corporation (ZEC), Faina Idarus Faina amesema,katika ziara yao ya mafunzo mwaka 2024 tija itaonekana kwa Wafanyakazi wa pande zote mbili za Muungano.

Alisema,licha ya wao kushughulika na suala la Nishati hiyo ya Umeme kwa kuwahudumia Wananchi wa Visiwa vya Zanzibar lakini walikosa kujua namna ambavyo Nishati hiyo muhimu imekuwa ikizalilshwa.

Faina aliendelea kusema kwamba, ziara hiyo imekuwa darasa muhimu kwao, kwani waweza kujifunza mambo wasiyoyajua huku wakiimarisha uhusiano na wafanyakazi wenzao wa Tanzania bara.

Alisema,elimu waliyopata itawasaidia katika kuwaelimisha wateja wanaowahudumia pindi wanapolalamikia mambo ambayo hayakutokea kwa makusudi ila ni changamoto za kitaalam.

"Tumejua mengi ambayo hatukuwahi kuyajua,sie tumekuwa tukinunua umeme Tanzania bara kwa bulk na tunauza kwa wananchi"alisema Faina na kuongeza.

"Ziara yetu tumejifunza mengi,tumeimarisha uhusiano sasa tutatatua mambo mengi kwa wakati mmoja...pia tumepata elimu tutawaelimisha wateja wetu pindi wanapopiga yowe kukatika kwa umeme maana huwa sio kusudi"alisema Faina. 

Naye Kaimu Meneja wa Vituo vya kuzalisha Nishati ya Umeme Pangani Hydro Syestem, Kulwa Sosthenes alisema, wafanyakazi hao wa ZECO wametembelea vituo vya kuzalisha umeme wa nguvu ya maji New Pangani Force.

Sosthenes alisema kwamba,wageni hao wamejifunza jinsi umeme unavyozalishwa huku wakifahamiana na wenzao wa Tanzania bara hatua ambayo anaamini itaimarisha mahusiano na pia kuleta tija maeneo ya kazi.

Katika siku ya kwanza ya ziara yao Jijini Tanga,wakiwa wameambatana na Mbunge wa Jimbo la Amani Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar, Abdul Yusuph Maalim, aliishauri Serikali kutenga fedha kwa ajili ya ziara za mafunzo kwa wafanyakazi wa taasisi. 

Mwisho. 



 Pichani ni mkuu wa kituo cha Hale Pangani  Hydro  Syestem,Kulwa Sosthenes akiwa ofisini kwake mara baada ya kuwapokea wafanyakazi wa shirika la umeme  ZECO Zanzibar.



Pichani ni kocha wa timu ya Soka ya Tanesco Tanga,Chausa Mganga akitangaza kuifua kikosi chake.

Kocha wa timu ya Soka ya Tanesco Tanga,Chausa Mganga ameahidi kuongeza makali mwaka 2024 kwenye kikosi chake hatua ambayo itawawezesha kupata ushindi mnono dhidi ya wapinzaji wake ambao watashuka dimbani kucheza michezo mbali mbali ikiwemo na ZECO kutoka Visiwani Zanzibar.


Chausa ametoa Matambo hayo Jiiini Tanga mara baada ya michezo ya Kirafiki dhidi ya Tanesco ya Zanzibar na matokeo ya mtanange huo uliopigwa Viwanja vya Popatlal yalikuwa mabao 2-2.

Baada ya michezo hiyo uliokuwa na upinzani mkali uliofanikiwa kuteka mashabiki wengi kutoka ndani ya Jiji la Tanga Viongozi wa timu zote mbili waliowapa fursa ya kutoa maoni yao.

Meneja wa Shirika la Umeme Tanesco Mkoani Tanga,Mathias Solongo aliyekuwepo kwenye mchezo huo alisema,licha ya kukubaliana na matokeo ya mchezo huo.lakini anaamini Vijana wake wangeweza kupata matokeo mazuri zaidi.

Alisema,vijana wake chini ya Mwalimu wao Chausa Mganga walionesha mchezo mzuri ikiwa ni ishara kwamba wameyaelewa mafunzo waliyopew na Mwalimu wao.

Hata hivyo,alisema kuwa pengine kilichowasababisha kupata sare hiyo ni kasoro ndogo ndogo ambazo sasa zitakwenda kufanyiwa kazi na kuwawezesha kupata ushindi kwa kila mchezo.

Ili waweze kufanya vyema kwenye michezo yao, Mhandisi Solongo alisema atahakikisha vijana hao wanapata maandalizi maazuri yatakayowawezesha kupata ushindi mchezoni.

"Timu yangu ni nzuri na niseme tu tutaendelea na.maandalizi ya kujiwinda kwa mchezo wa marudiano,nasi tutatafuta nafasi ya kuwafuata kule Zanzibar"alisema Solongo huku akiahidi kwenda kipata ushindi.

Naye Kiongozi wa timu ya Shirika la umeme Zanzibar Electricity Corporation (ZECO), alisema kwamba,hakuna ushindi wa kirahisi utakaopatikana kutoka kwa Vijana wake.

Alijinadi kuwa timu yake ni bora na Tanesco Tanga wajiandae kupogea kipigo pindi watakapokanyaga ardhi ya Visiwa vya Zanzibar. 

Pamoja na hayo pia alielezea kuridhishwa kwake na mapokezi mazuri waliyopata kutoka kwa wenyeji wa Tanesco Tanga akisema wamefarijika kwa ujarimu na ushirikiano waliopata.

Alisema kuwa,ziara hiyo ya michezo imewawezesha kujifunza mambo mbalimbali hatua ambayo itasaidia kuongeza ufanisi kwenye majukumu yao ya kazi. 

Mwisho.

 

No comments:

Post a Comment