Tuesday, 17 March 2026

WADAU WA MASHINDANO YA DUVII RAMADHANI CUP 2026 KASERA YATUMIKA KUINUA UCHUMI KWA WAJASIRIA MALI,,,


Picha ni Mratibu wa mashindano hayo,Gidion Zumba amesema kuwa mashindano ya Duvii Ramadhani Cup 2026 kusaka washindi mbalimbali huku kufanyika usiku wilayani hapo,lengo kusaka washindi watatu ambao watapata medani na pesa tasilimu.

Na Sophia Wakati,Mkinga

TIMU za soka 48 zimejitokeza wilayani Mkinga mkoani Tanga kushiriki mashindano ya Duvii Ramadhani CUP 2026 kuwania zawadi mbalimbali ikiwemo pesa tasilimu.

Mratibu wa mashindano hayo,Gidion Zumba amesema kuwa mashindano hayo ambayo niya kwanza kufanyika usiku wilayani hapo,lengo kusaka washindi watatu ambo watapata medani na pesa tasilimu.

Alisema kwamba mshindi wa kwanza katika mashindano hayo atakabiziwa pesa tasilimushilingi million 2,000,000,mshindi wa pili million 1,000,000 na watatu 500,000 .

Aidha alibainisha kueleza kwamba zawadi nyingine   ni mchezaji bora shilingi 200.000,mfungaji bora shilingi 200,000 na kipa bora 100,000 sambamba na kupatiwa medani.

Mratibu Zumba alisema kuwa mashindano hayo yanafanyika usiku katika uwanja wa soka Kasera  wilayani hapo kwa mtindo wa mtoano.

'' Mashindano haya yalipangwa kufanyika mwaka jana kwa kuweka maandalizi ya uwanja,lakini kutokana na kujitokeza sababu mbalimbali ilishindikina na kupelekea kufanyika mwaka huu 2026''alisema Mratibu huyo Zumba.

Mratibu Zumba alisema mashindano mbalimbali yamewahi kufanyika katika tarafa mbalimbali yakifahamika kwa jina la Samia Mkinga Cup 2025 ambayo yalishirikisha timu 126 washindi walipata mnyama ng'ombe, mbuzi,jezi na pesa tasilimu.

Katika mashindano hayo yakiendelea kufanyika timu shiriki katika mashindano hayo, zimekuwa zikinufaika na jezi,mipira na pesa tasilimu 100,000 ikiwa ni sehemu ya maandalizi.

Alisema michuano hiyo ya Samia Cup ambayo yalisaidia kupata timu nane bora kila tarafa ambapo walipatikana mshindi alipata shilingi 1,000,000 na ng'ombe,wa pili mbuzi na 500,000 huku wa tatu akizawadiwa 300,000 na mshindi wanne 100,000.

Hata hivyo,Mratibu Zumba alisema michezo ni muhimu sana kwani husaidia vijana kuweza kujiajiri,kupata kipato na kuweza kuondokana na kujiingiza kwenye makundi hatarishi kupoteza ndoto zao.

''Mashindano ya Duvii Ramadhani Cup hayana kiingilio hivyo amewataka vijana kutumia fursa hiyo kuonyesha vipaji vyao ili kuweza kuonekana''alisema Mratibu huyo Zumba.
Mwisho.


Na Sophia Wakati,Mkinga
WADAU wa michezo Kasera wilayani Mkinga wamempongeza mdhamini wa mashindano ya Duvii Ramadhani Cup ambayo yanasaidia kuleta faraja kwa wananchi.

Mwenyekiti wa Timu ya Soft Toch yenye masikani yake Kasera wilayani Mkinga,Said Kassim amesema michuano hiyo imekuwa mkombozi kuamsha ari kwa jamii.

Amesema kwamba timu hiyo imeshirikisha vijana kutoka maeneo mbalimbali ya Mkinga lengo kuonyesha vipaji na kuwania zawadi zilizopo.

Said amesema mashindano hayo ambayo yanafanyika usiku niya kwanza yametokea kukubalika kwa wadau ikiwemo vilabu.

''Mashindano ya Duvii Ramadhani Cuo 2026 yameweza kusaidia kuonyesha vipaji mbambali vya michezo vilivyopo wilayani Mkinga kwani tumekuwa tukishuhudia mashindano ya usiku maeneo mengine.

''Kwa mashindano haya tunampongeza mdhamini wa mashindano haya Duvii na muandaaji wake Zumba kuleta burudani hizi kwa vijana kutoka wilaya ya Mkinga''alisema Mwenyekiti wa timu ya Soft Said.

Hata hivyo,amesema tayari vijana wamepata uzoefu na mechi za usiku pia amewataka wadau wa michezo kuendelea kumuunga mkono mdhamini na mwandaaji ili kuweza kuwa endelevu kufanyika wilayani hapo.
Mwisho.





Timu ya soka Mtundani imepata nafasi ya kusonga mbele mashindano ya Duvii Ramadhani Cup baada ya kuifunga wapinzani wao Veterani kwa kwa goli 1-0.

Mchezo huo wa mwendelezo wa vuta nikuvute kwa pazo zote kuonyesha vipaji vya mchezo wa soka,umefanyika saa 10 jioni katika uwanja wa soka Kasera uliopo wilayani Mkinga,

Mtundani imefanikiwa kuandika goli lake mnamo dakika ya 21 kupitia kinara wa timu hiyo,Athumani Mwarasi ambalo limeweza kudumu mpaka dakika 90 mwisho wa mchezo huo.
Mwisho.


Mwenyekiti wa kitongoji Kasera,Rajabu Juma amesema mashindano ya Duvii Ramadhani Cup yamekuwa chachu kwa kina kuyatumia kufanya biashara mbalimbali.

Amesema Wakinamama wananufaika kufanya biashara ndogondogo kwa kiwango kikubwa na hufanyika muda mzuri usiku ambapo niyakwanza kufanyika na kuwavutia wadau wengi.


Pia ametumia nafasi hiyo kumuomba mdhamini wa mashindano hayo Rashid Duvii kuwa endelevu kufanyika kila mwaka ili wananchi waweze kufanya biashara na vijana kuweza kuibua vipaji vyao.

Mwenyekiti huyo wa kitongoji,Rajabu ameomba kufanyika maboresho ya kiwanja hicho ili kuwezesha kuzishu 

Sunday, 19 October 2025

MGOMBEA UBUNGE CCM,NJAMA MPENI KURA ZA KISHINDO MGOMBEA URAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSANI KULIPA FADHILA,,

 Picha ambaye ameshika kipaza sauti ni.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Korogwe Mjini kupitia CCM, Charles Njama amesema, Mgombea urais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweza kutekeleza miradi mengi mingi ya maendeleo ya Wananchi hivyo kuna kila sababu ya kulipwa mema kwa kupigiwa kura nyingi za kishindo.


Njama ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Kwamsisi,amesema Rais Dkt Samia ametoa fedha nyingi kwenye Kata hiyo kwa ajili ya miradi ya maendeleo hivyo akipatiwa Kura nyingi kwenye uchaguzi ujao itamsukuma kuongeza kasi ya kusukuma miradi mingi kwa wananchi .

'' Ikifika Oktoba 29 mjitokeze kwenda kupiga kura,tena muwashawishi na kuwahimiza wenzenu wengine kwenda kupiga kura,tukampe kura nyingi za kishindo Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ''alisema mgombea huyo wa ubunge Jimbo la Korogwe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM.

Mbali na hayo Njama alisema kwamba,atakapoingia madarakani miongoni mwa vipaumbele vyake ni pamoja na kushirikiana na vijana katika kuinua uchumi kwa kuwawezesha mitaji sanjari na matumizi ya sekta ya michezo na sanaa kuongeza kipato.

Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya sita imetoa fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo ya Wananchi huku akitaja ujenzi mradi wa Kilimo cha umwagiliaji kwa wakazi wa Kata ya Kwamsisi, mradi ambao utasaidia kukuza uchumi kwa wananchi.

''Shilingi bilioni 24.5 zimeletwa na Rais Dkt Samia kwa ajili ya bonde la kilimo.Kupitia bonde hili mtalima na kuvuna kwa wingi na kuuza kwenye soko la ndani na hata nje''alisema Njama huku akishangiliwa na Wananchi waliohudhuria mkutano huo wa kampeni.

Aidha Njama alisema,pindi mradi huo utakapoanza kutekelezwa atahakikisha kwamba kipaumbele cha ajira hususani zile za muda wanazungumza na kukubaliana na mkandarasi ili shughuli hiyo kupewa wenyeji.


Picha ni Mgombea wa kata ya Kwamsisi wilayani Korogwe,Nassoro Mohamed akiwa kwenye mkutano wa kampeni, akimuombea Kura Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akisema ni Kiongozi aliyefanikiwa kutekeleza ilani ya CCM kwa asilimia 100.
Picha ni Mjumbe wa kamati ya siasa ya Korogwe Mjini,Omari Mahanyu akizungumza kwenye mkutano wa kampeni shule ya msingi Kwakombo kata ya Kwamsisi alisema,Wananchi wanakila sababu kuwachagua wagombea wanaotoka Chama Cha Mapinduzi CCM kwa maelezo kuwa ndicho chenye Ilani inayotekelezeka.

Aidha,amewasihi Wananchi wa Kata ya Kwamsisi kuhakikisha kwamba ifikapo Oktoba 29 mwaka huu wanamchagua Rais Dkt Samia Suluhu, Mbunge Charles Njama na diwani Nassoro Mohamed.
Pichani ni mashabiki wakiburudika kwenye mkutano wa kampeni wa CCM.






BIRUMO''VIJANA WA CCM TUMEJIPANGA KULINDA NCHI,,,,



  • Picha ni Mwenyekiti wa Vijana wa CCM Jimbo la Korogwe Mjini,Moses Birumo katika mkutano wa kampeni akiwataka Vijana kutokuwa Chanzo cha kuharibu amani ya nchi.

MWENYEKITI wa Vijana wa CCM Korogwe Mjini,Moses Birumo amewataka Vijana kutokuwa Chanzo cha kuharibu amani ya nchi badala yake amewasihi kuwa mstari wa mbele katika kuilinda Amani.

Birumo ametoa kauli hiyo jana katika mkutano wa hadhara wa kampeni kuwanadi wagombea wa chama cha Mapinduzi CCM uliofanyika Kata ya Magunga iliyop Korogwe Mkoani Tanga.

Katika mazungumzo yake kwa wananchi,Birumo alisema: '' Vijana hatuwezi kuwa chanzo cha kuharibu amani ya nchi, tutailinda amani kwa nguvu zote'' alisema Mwenyekiti huyo wa Vijana Moses Birumo. 

Katika mkutano huo wa kamepni alitumia nafasi hiyo kuwaasa vijana kutokubali kurubuniwa na baadhi ya watu wenye Nia ya kuvuruga amani huku akiwataka kuhakikisha kwamba ifikapo Oktoba 29 mwaka huu wanapiga kura.

Kwa upande wake mgombea Udiwani wa Magunga, David Mbwilizi aliwaeleza Wananchi kwamba CCM ndio chama pekee chenye uwezo wa kuharakisha maendeleo ya Wananchi wa Tanzania.

Kutokana na hali hiyo aliwaomba wananchi wa kata ya Magunga kuhakikisha kwamba wanapiga kura nyingi kwa Chama Cha Mapinduzi wakimchagua mgombea wa nafasi ya uRais,Ubunge pamoja na madiwani wa chama hicho.

Kwa mujibu wa mgombea Udiwani kata ya Magunga kupitia,David Mbwilizi,amesema wananch kuipa ridhaa CCM kuendelea kushika dola kutawezesha kufanikisha utekelezwaji wa miradi mingi ya maendeleo kwenye maeneo yao. 

Kwa upande wa sekta ya afya ,Mgombea Mbwilizi alisema, pindi chama hicho kufanikiwa kuingia madarakani kupitia Ilani iliyopo watahakikisha kunajengwa Zahanati za kutosha kwa lengo la kupunguza mzigo kwa hospitali ya Magunga. 

Mbali na hayo Mbwilizi ameishukuru Serikali ya Chama Cha Mapinduzi CCM kwa kuwezesha upatikanaji wa huruma za nishati ya umeme kwenye maeneo mengi na hivyo kuharakisha maendeleo ya Wananchi wa Korogwe. 

Hata hivyo,alisema,ni imani yake kwamba Wananchi wakikichagua Chama hicho tawala itakuwa rahisi kwa maeneo wachache yaliyosalia kufikishiwa huduma ya umeme kuweza kuondoa changamoto hiyo. 
Mwisho.



Pichani ni vikundi mbalimbali vya sanaa vikiburudisha katika mkutano wa kampeni kata ya Magunga wilayani Korogwe.

Saturday, 18 October 2025

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KOROGWE MJINI''CHARLES NJAMA AWAOMBA WANANCHI OKTOBA 29 CHAGUENI WAGOMBEA WA CCM KUHARAKISHA MAENDELEO,,


Picha ni Mgombea Ubunge wa Jimbo la Korogwe Mjini kupitia chama cha Mapinduzi CCM,Charles Njama akiomba kura kwa wananchi huku akiwaeleza wananchin sifa za Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweza kutekeleza miradi mingi ya maendeleo.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Korogwe Mjini kupitia chama cha Mapinduzi CCM,Charles Njama amesema,Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweza kutekeleza miradi mingi ya maendeleo hivyo kuna kila sababu ya kulipwa mema kwa kupigiwa kura nyingi za kishindo.
Njama ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika shule ya msingi Kwakombo kata ya Kwamsisi iliyopo Korogwe mkoani Tanga,,amesema Rais Dkt Samia ametoa fedha nyingi kwenye Kata hiyo kwa ajili ya miradi ya maendeleo hivyo akipatiwa Kura nyingi kwenye uchaguzi ujao itamsukuma kuongeza kasi ya kusukuma miradi mingi kwa wananchi .

'' Ikifika Oktoba 29 mjitokeze kwenda kupiga kura,tena muwashawishi na kuwahimiza wenzenu wengine kwenda kupiga kura,tukampe kura nyingi za kishindo Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ''alisema mgombea huyo wa ubunge Jimbo la Korogwe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM.

Mbali na hayo Njama alisema kwamba,atakapoingia madarakani miongoni mwa vipaumbele vyake ni pamoja na kushirikiana na vijana katika kuinua uchumi kwa kuwawezesha mitaji sanjari na matumizi ya sekta ya michezo na sanaa lengo kuongeza kipato.

Aidha aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya sita imetoa fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo ya Wananchi huku akitaja ujenzi mradi wa Kilimo cha umwagiliaji kwa wakazi wa Kata ya Kwamsisi, mradi ambao utasaidia kukuza uchumi kwa wananchi.

''Shilingi bilioni 24.5 zimeletwa na Rais Dkt Samia kwa ajili ya bonde la kilimo.Kupitia bonde hili mtalima na kuvuna kwa wingi na kuuza kwenye soko la ndani na hata nje''alisema Njama huku akishangiliwa na Wananchi waliohudhuria mkutano huo wa kampeni.

Aidha Njama alisema,pindi mradi huo utakapoanza kutekelezwa atahakikisha kwamba kipaumbele cha ajira hususani zile za muda wanazungumza na kukubaliana na mkandarasi ili shughuli hiyo kupewa wenyeji.

Amewasihi Wananchi wa Kata ya Kwamsisi kuhakikisha kwamba ifikapo Oktoba 29 mwaka huu wanamchagua Rais Dkt Samia Suluhu, Mbunge Charles Njama na diwani Nassoro Mohamed.

Mwisho.

Pichani ni Mgombea Udiwani kupitia Chama cha Mapinduzi CCM kata ya Kwamsisi,Nassoro Mohamed  alitumia wasaa huo kumuombea Kura Rais Dkt Samia Suluhu Hassan akisema ni Kiongozi aliyefanikiwa kutekeleza ilani ya CCM kwa asilimia 100.


Pichani ni miongoni mwa wasanii wa kikundi cha kwaya wakionyesha burudani katika mkutano wa kampeni za chama cha Mapinduzi CCM kuwanadi Wagombea wake.




Friday, 26 September 2025

MKUTANO WA WAGOMBEA UBUNGE NA UDIWANI KATA YA NGAMIANI KUSINI JIJINI TANGA ILIKUWA HIVI,,,

Pichani ni Mgombea Ubunge wa chama cha Mapinduzi CCM Jimbo la Tanga Mjini, Kassim Amary Mbaraka, akiwaeleza wananchi wa Ngamiani kusini, pindi mkinipatia ridhaa, atakwenda kusimamia ujenzi wa barabara 'Ring road' itakayotumika na magari makubwa 'malory' ikipita nje ya Mji kwa lengo la kuepusha msongamano kutoka maeneo ya Bandari.

MGOMBEA Ubunge wa chama cha Mapinduzi CCM Jimbo la Tanga Mjini, Kassim Amary Mbaraka, amesema kwamba, pindi wananchi wakimpatia ridhaa, atakwenda kusimamia ujenzi wa barabara 'Ring road' itakayotumika na magari makubwa 'malory' ikipita nje ya Mji kwa lengo la kuepusha msongamano kutoka maeneo ya Bandari.

Mbarak almaarufu Makubel ameyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Ngamiani Kusini katika halmashauri ya Jiji la Tanga, huku aliwasihi wananchi kumpatia kura nyingi Rais atokanaye na CCM, yeye Mbunge na madiwani wake.

Katika mkutano huo wa kampeni, Makubel alisema kwamba, mgombea urais wa CCM Dk. Samia kutua Tanga amekusudia kuifanyia Tanga mambo makubwa mazuri kwa wananchi.

Makubel  ametaja mambo hayo kuwa ni pamoja na utekelezwaji ujenzi wa miundombu ya barabara kutoka Bandarini kupitia nje ya Mji ambayo itatumiwa na malori hatua ambayo itasaidia kupunguza msongamano.

"CCM imekusudia kuifanyia Tanga mambo makubwa, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amekusudia makubwa,kutajengwa 'ring road' kuingia na kutoka Bandarini,mkinichagua nitaenda kulisimamia hili" alisema Kassim Amary Mbaraka almaarufu Makubel.

Kwa mujibu wa Makubel miradi mingine inayoenda kutekelezwa Tanga iwapo Serikali ya CCM itapata ridhaa kuingia madarakani ni ujenzi wa reli ya SGR kutoka Tanga, Kilimanjaro,Arusha hadi Singida na ujenzi wa uwanja wa ndege uliyo wa kisasa.

Mbali na hayo, Makubel alisema, iwapo Wananchi watawachagua Rais ,Mbunge na Madiwani wa CCM na kuwawezesha kushika dola jitihada mbalimbali zitafanyika ili kufufua Viwanda hatua ambayo itafufua Uchumi wa Tanga.

Aidha Mgombea Udiwani kupitia CCM Kata ya Ngamiani Kusini, Mtanga Aweso alisema,kilichomsukuma kuwania wadhifa huo kwa awamu nyingine ni kwa vile Ilani ya Chama chake imetekelezwa kikamilifu.

Mtanga amejivunia kufanikiwa kwenye usimamizi upatikanaji wa mikopo kwa Wanawake ,Vijana na walemavu ambapo kwenye nyanja ya elimu alisema ameweza kusukuma upatikanaji wa shule yenye ghorofa ndani ya kata yake.

Awali Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM wilayani Tanga, Meja mstaafu Hamisi Mkoba alimuombea kura mgombea uRais wa CCM Dk. Samia Suluhu Hassan akisema,ni Kiongozi aliyemudu kusimamia haki, umoja na mshikamano, aliwasihi wananchi kuwachagua wagombea wa Chama tawala.
Mwisho.





 Pichani katikati mwanamke ambaye amevaa kilemba na sare ya CCM ni Mgombea Udiwani kupitia CCM Kata ya Ngamiani Kusini, Mtanga Aweso akiwasili eneo la mkutano akisindikizwa na wananchi wa kata hiyo.

Friday, 12 September 2025

UZINDUZI WA KAMPENI JIMBO LA KOROGWE MJINI ILIKUWA HIVI,,,


 Picha mkono wa kulia ni Mwenyekiti wa CCM Jimbo la Korogwe Mjini,Thobias Nungu  akiwataka Wananchi kupiga kura nyingi za heshima kwa mgombea Urais Dk. Samia Suluhu Hassa,madiwani huku akimnadi Mgombea  Ubunge wa Jimbo la Korogwe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),Charles Njama (kushoto ambaye anawasalimia wananch) hafla iliyofanyika katika uzinduzi wa kampeni uliofanyika uwanya wa Manundu sokoni uliopo wilayani hapo.





Pichani ni Katibu wa Chama cha Mapinduzu CCM jimbo la Korogwe mjini,Evarts Mluge akiwahutubia wananchi wa Korogwe akiwanadi mgombea Urais Dk. Samia Suluhu Hassan Mbunge na madiwani.




Pichani ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi wilaya ya Korogwe mjini,Mujibu Wandi,akiwataka wananchi kuchagua wagombea wa chama cha mapinduzi ili kuendelea kuleta maendeleo.


MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Korogwe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),Charles Njama akiomba wananchi kupiga kura nyingi kwa wagombea wa Chama tawala huku akiahidi kwamba kwa kufanya hivyo kutatoa fursa uwepo wa Korogwe ya Viwanda.




 
Pichani juu ya bajaji ni MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Korogwe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),Charles Njama akiwasili katika uwanja wa Manundu sokoni hafla ya uzinduzi kuwanadi wagombea wa Chama tawala .

Wednesday, 10 September 2025

UWT KOROGWE MJINI WAJITOKEZA KUFANYA USAFI MAANDALIZI UZINDUZI WA KAMPENI KUWANADI WAGOMBEA WAKE,,,

Pichani ni Katibu wa Umoja wa wanawake (UWT)Korogwe Mjini,Suzana Mandia akitoa maelezo mpango mkakati uliopo katika maandalizi ya uzinduzi wa kampeni kuwanadi wagombea wa CCM ili kuwezesha kupata kura za kishindo,alitoa kauli hiyo katika zoezi la kufanya usafi uwanja wa sokoni uliopo kata ya Manundu. wilaya ya Korogwe mkoa wa Tanga.