Pichani ni katibu tawala wa wilaya ya Korogwe,Rehema Said Bwasi aliyemwakilisha mkuu wa wilaya hiyo,Mhandisi Robert Gabriel. akifungua mradi wa maji juzi kata ya Lutindi wilayani hapo.
NA SOPHIA
WAKATI,KOROGWE
WANANCHI wa
vitongoji vya Nazareth juu na Gombelo huko kata ya Lutindi wilayani Korogwe
wameondokana na kero ya kutembea umbali mrefu kusaka maji baada ya mradi
uliogharimu kiasi cha sh 7 milioni kukamilika.
Mradi huo
ambao umezinduliwa juzi na katibu tawala wa wilaya ya Korogwe,Rehema Bwasi
aliyemwakilisha mkuu wa wilaya hiyo,Mhandisi Robert Gabriel.
Baada ya
kuzindua mradi huo wa jamii uliojengwa kwa ufadhili wa mtawala wa hospitali ya
magojwa ya akili kwa kushirikiana na wananchi katibu tawala alihimiza utunzaji
mazingira na misitu katika vyanzo vya maji.
Alisema, ili
mradi huo kuwa endelevu kwa maslahi ya vizazi vya sasa na vijavyo wananchi
hawana budi wanapaswa kuepuka vitendo vya uharibifu wa mazingira kwa kukata
miti ovyo ama kuchoma misitu.
Alitumia
wasaa huo kumpongeza mtawala wa hospitali hiyo ya Lutindi,Tim Hammerbacher kwa
hatua yake kusaidia huduma za jamii kuondoa kero hiyo ya maji.
Awali akisoma
taarifa ya mradi huo kwa mgeni rasmi Afisa mtendaji wa kijiji cha
Lutindi,Gerdath Nyangasa alisema mfadhili huyo amechangia sh 5 milioni kwa
ajili ya ununuzi wa vifaa na kulipia ufundi.
Aidha afisa
huyo,alisema kwamba wananchi wakiwa wamechangia nguvu kazi ikiwemo kuchimba
mitaro ambayo ni sawa na sh 2 milioni hivyo kufanya jumla ya sh 7 milioni
za kitanzani kuwa gharama halisi ya mradi.
Vilevile
afisa huyo alibainisha kwamba familia ya mzee Elikana Madeni imetoa eneo lao
kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa tenki la kuhifadhia maji lenye uwezo wa
kubeba lita 20,000.
Nae diwani
wa kata ya Lutindi,Nicolas Shemsanga alisema, ingawa mradi huo ulilengwa kwa
vitongoji viwili lakini una uwezo wa kuhudumia vitongoji zaidi ya hivyo.
Pia,alitumia
nafasi hiyo kumpongeza mfadhili ambaye ni mtawala wa hospitali ya magonjwa ya
akili Lutindi, Tim Hammerbacher akimweleza kuwa amekuwa na msaada mkubwa
kujitolea kwenye huduma za jamii akitolea mfano barabara.
Mwisho.
Pichani ni katibu tawala wa wilaya ya Korogwe,Rehema Said Bwasi aliyemwakilisha mkuu wa wilaya hiyo,Mhandisi Robert Gabriel. juzi mara baada ya kufungua mradi wa maji kata ya Lutindi wilayani hapo akimtwika mkazi wa Gombero ndoo ya maji..
No comments:
Post a Comment