Sunday 15 October 2017

ZIARA YA WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA NA TEKNOLOJIA PROF. JOIYCE NDALICHAKO ILIKUWA HIVI KOROGWE,,,


 Pichani wa pili mkono wa kushoto ambaye anatabasamu ni Waziri wa elimu Sayansi na teknolojia Profesa Joyce Ndalichako mara baada ya ziara yake wilayani Korogwe mara baada ya kufungua na kuweka jiwe la msingi miradi ya shule.,


Pichani wa pili mkono wa kushoto ambaye anaongea ni Waziri wa elimu Sayansi na teknolojia Profesa Joyce Ndalichako mara baada ya ziara yake wilayani Korogwe,akizungumzia mpango uliopo kwa serikali kwamba hadi kufikia mwaka 2020 hakutakuwa na shule yenye vyumba vya madarasa vya nyasi,kushoto mwanaume ni mkuu wa wilaya hiyo,Mhandisi Robart Gabriel,wa tatu ni mbunge wa jimbo la Korogwe mji,Mery Chatanda akifuatiwa na mkurugenzi wa halmashauri ya Korogwe mji,Jumanne Shauri kulia..



NA SOPHIA WAKATI,KOROGWE
WAZIRI wa elimu Sayansi na teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amesema kwamba hadi kufikia mwaka 2020 hakutakuwa na shule yenye vyumba vya madarasa vya nyasi.

Profesa Ndalichako ameyasema hayo juzi katika ziara yake ya siku moja wilayani Korogwe alikotembelea kufungua na kuweka jiwe la msingi baadhi miradi ya shule za halmashauri ya Korogwe Mjini. 

Alisema, kwa kasi ambayo inaendelea kwenye uboreshaji miundombinu ya sekta ya elimu ili kuwawezesha watoto kupata elimu itakayokuwa na ubora unaokubalika. 

Profesa Ndalichako alitumia fursa hiyo kupongeza jitihada za ujenzi zilizoonyeshwa wilayani Korogwe akitaka mshikamano huo kuendelea kuwepo kati ya Viongozi na wananchi. 

"Kumekuwa na propaganda za kuwakatisha wananchi tamaa, ila niwaombe endeleeni kumuunga mkono rais Dk.John Pombe Magufuli na kushirikiana nae na lazima muelewe wananchi mnayo nafasi kuchangia maendeleo yenu "alisema. 

Aidha Profesa Ndalichako aliongeza kwa kubainisha kuwa rais Dk. John Magufuli anapenda watu wanaojituma na kwa aliyoyaona Korogwe hatosita kumfikishia salaam. 

Aidha, aliwataka walimu kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia weledi na kuwajengea uzalendo watoto hatua itakayowawezesha kupenda nchi yao. 

Pia,ametumia nafasi hiyo kuwaasa wanafunzi kutokubali kutoa fursa kwa watu ambao kila uchao wamekuwa wanawaza kupoteza amani ya nchi ambayo imekuwa gumzo kwa miaka mingi. 

Katika ziara hiyo ya Profesa Ndalichako, mkuu wa wilaya ya Korogwe Mhandisi Robert Gabriel alimweleza Waziri huyo kuwa, Korogwe imejidhatiti kufanya kazi badala ya kuruhusu migogoro. 

"Kiukweli Korogwe tunataka kazi ndio ziongee, hatutaki maneno na nikuahidi mheshimiwa Waziri sisi tutaendelea kuchapa kazi "alisema mkuu huyo wa wilaya ya Korogwe. 

Vilevile mkuu huyo wa wilaya alimweleza Waziri kuwa jitihada za ziada zimekuwa zikifanyika kufanikisha ujenzi wa mabweni ili kuwaondoshea changamoto watoto wa kike. 

"Ukimlinda mtoto wa kike utakuwa umelinda Taifa, tumeamua kumpa mtoto wa kike elimu na tunajenga mabweni ili kuwawezesha kutimiza hatma yao ambayo pia ni hatma ya Taifa "alisema DC Mhandisi Gabriel. 

Wakati akizindua bweni kwa shule ya Sekondari Semkiwa Profesa Ndalichako aliahidi kufanya kila liwezekanalo kupata magodoro ili kuwawezesha watoto kuyatumia mabweni hayo haraka iwezwkanavyo akiahidi sh 10 mil. 
Mwisho. 

No comments:

Post a Comment