wiki ya miaka 13 tangu kuanzishwa kwa TPA kwa sheria
namba 17 ya mwaka
2004 ya usimamizi wa Bandari.na kushoto ni Meneja
wa bandari mkoa wa Tanga,Percival Salam
Wadau wa bandari mkoani Tanga wakiwa kwenye kikao
Pichani ni boti mpya ya kisasa ya ulinzi iliyogharimu sh.billion nne za kitanzania kwa ajili ya ulinzi mizigo ya magendo bahari ya Hindi, juzi miongoni mwa shughuli zilizofanyika katika.
wiki ya miaka 13 tangu kuanzishwa kwa TPA kwa sheria
namba 17 ya mwaka
2004 ya usimamizi wa Bandari.
Pichani ni Meneja wa bandari mkoa wa Tanga,Percival Salama mara baada ya kamilika kwa zoezi la michezo wakijipongeza kwa pamoja.
Pichani ambaye ametangulia ni Meneja wa bandari mkoa wa Tanga,Percival Salama akiwa ameambatana na wafanyakazi na wadau wa habari Siku ya kuhitimisha sherehe ya wiki ya bandari miaka 13 tangu kuanza kutoa huduma.
NA SOPHIA WAKATI,TANGA
MAMLAKA ya usimamizi wa bandari mkoani Tanga TPA,imesema ina mpango mkakati wa kuhudumia kiasi
cha shehena ya mizigo tani millioni 2 kwa mwaka ifikapo mwakani baada ya
kuwasili kwa mashine mpya za kupakua na kupakia mizigo melini.
Meneja
wa bandari mkoa wa Tanga,Percival Salama alisem kwamba katika
utekelezaji wa wa ahadi ya rais Dk.John Pombe Magufuli kuna mashine
mbili za kisasa
zinatarajiwa kuwasili nchini mwezi Machi na zitafungwa kwa ajili
ya kuboresha utoaji huduma katika bandari hiyo.
Alisema
kwamba pia hivi sasa uwezo wa bandari hiyo ni mkubwa kuhudumia shehena ya mizigo kiasi
cha tani 750,000 kwa mwaka kutoka tani 548,000 katika kipindi cha mwaka
2015 kuhudumia shehena hiyo.
Meneja
huyo alitaja mafanikio ya uhudumiaji mizigo kwa bandari hiyo tangu
mwaka 1960 ambapo waliweza kuhudumia shehena ya mizigo ipatayo tani
212,000 ilipanda na kufikia tani 380,000 mwaka 1975.
"Kiukweli sasa tunafanya
maboresho ya uhakika katika bandari yetu, kwa kufunga mashine mpya
mbili za kushusha mizigo na kupakia melini lakini pia tutakuwa na Tag
zitakazoweza kubeba tani 100 kwa wakati mmoja," alisema meneja huyo Salama.
Aidha abainisha
kueleza kwamba uwepo wa bandari ya Tanga inaumuhimu mkubwa kwa ukuaji
wa uchumi mkoani humo na pia ni fursa nzuri kwa wafanyabiashara
wa ndani na nje ya nchi kupitisha mizigo yao kwa kuwa inahudumiwa katika muda mfupi kuliko
bandari yoyote hapa nchini.
Salama
alitaja miongoni mwa nchi ambazo zinaweza kuhudumiwa moja kwa moja na bandari
hiyo kuwa ni ile ya Zambia, Malawi, DR Congo, Rwanda, Burundi, Uganda na nchi jirani ya Kenya
kupitia miundombinu bora ya reli na barabara.
Mkuu wa wilaya ya Tanga, Thobias Mwilapwa akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Tanga,Martin Shigela katika uzinduzi wa
wiki ya miaka 13 tangu kuanzishwa kwa TPA kwa sheria namba 17 ya mwaka
2004 ya usimamizi wa Bandari.
Alisema kwamba aliipongeza bandari hiyo kwa jitihada za kuongeza ufanisi mzuri wa kazi wanaofanya katika kuhudumia shehena za mizigo na ushirikiano na vyombo vyengine vya dola udhibiti suala la magendo kwa njia ya bahari.
Alisema kwamba aliipongeza bandari hiyo kwa jitihada za kuongeza ufanisi mzuri wa kazi wanaofanya katika kuhudumia shehena za mizigo na ushirikiano na vyombo vyengine vya dola udhibiti suala la magendo kwa njia ya bahari.
"Mamlaka ya bandari maboresho
mnayoyafanya yana mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi, na hii ndiyo
maana serikali kuu imekuwa ikitoa fedha lengo kuhakikisha uboreshaji unafanyika," alisema DC Mwilapwa.
Mkuu
huyo wa wilaya alisema jitihada zinazofanywa na bandari hiyo
katika kudhibiti bidhaa za magendo zinazopita katika bandari bubu zilipo
kwenye mwambao wa bahari ya Hindi na akaahidi mkoa umeanza kuchukua
hatua kupambana na magendo.
"Mkuu
wa mkoa ameagiza kwamba zilebidhaa za shehena ambazo tutakuwa tunakamata na chombo zaidi ya
Mara tatu magendo itabidi viongozi wa maeneo hayo watakuwa hawatoshi kuwepo,baada ya kujiridhisha wawajibike," alisema
Mwilapwa.
Pia alitoa wito kwa watu wanaotaka kuwekeza katika Jiji la Tanga kwamba
maeneo bado yapo na Halmashauri tayari imetenga eneo la Pongwe kwa ajili ujenzi
wa viwanda mbalimbali.
Hata hivyo,katika uzinduzi huo wa
wiki ya miaka 13 tangu kuanzishwa kwa TPA kwa sheria
namba 17 ya mwaka
2004 ya usimamizi wa Bandari wamefanikiwa kuchangia Uniti 27 za damu
kusaidia wagonjwa wenye mahitaji katika hospitali ya mkoa wa Tanga
Bombo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment