Sunday, 2 January 2022

KANISA LA KKKT LIMESEMA MWAKA 2022 UNA MATARAJIO MAKUBWA,WATANZANIA WANAPASWA KUANZA NA MUNGU,,,

 


 Pichani ni Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri KKKT Usharika wa Kana Dayosisi ya KaskaziniPwani, Masharik Ketto


NA SOPHIA WAKATI,TANGA

KANISA la Kiinjili la Kilutheri KKKT Usharika wa Kana Dayosisi ya
Kaskazini Mashariki limewataka Watanzania kuendelea kumrudia Mungu
hatua ambayo itawawezesha kuwa na mafanikio katika mwaka huu mpya wa 2022.

Hata hivyo,pia amewata viongozi waliopata nafasi ya kuitumikia jamii kuhakikisha wanafuata maadili na kutanguliza hofu ya mungu ili nchi iweze kufikia malengo yake.

Wito huo umetolewa juzi na Mchungaji Kiongozi,Thadeus Ketto wakati
akitoa Salaam za mwaka mpya kwa waumini wake ambapo alisema baada ya kuvuka salama 2021 mwaka 2022 ni mwaka wa matarajio makubwa na katika kuyafikia watanzania wanapaswa kuanza na Mungu.

Ketto ambaye pia ni Mkuu wa jimbo la Pwani alihimiza wananchi kufanya
kazi kwa bidii ili kujenga uchumi imara huku akiwasisitiza vijana
kuchangamkia fursa katika kujiimarishia kipato.

"Nitoe wito kwa jamii kwa ujumla wake tumtegemee Mungu zaidi,tufanye
kazi kwa bidii,vijana kuchangamkia fursa kama bomba la mafuta tuwe
wanufaika wa kwanza,tutajenga uchumi wa familia,jamii na nchi"alisema
Mchungaji huyo kiongozi Ketto.

Pamoja na hayo Ketto aliwasihi watanzania kufuata sheria na taratibu
zilizowekwa nchini ikiwa ni kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan
kumwezesha kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa katiba.

Mbali na hayo Mchungaji Ketto amehimiza upendo kwa kuhurumiana,kusaidia yatima,wanyonge na wazee sanjari na utoaji wa elimu kwa jamii ikiwa ni miongoni mwa matendo yanayompendeza Mungu.

Kwa mujibu wa Mchungaji Keto, KKKT ni Kanisa ambalo limekuwa na
ushirikiano mkubwa na Serikali kuhakikisha linaifikia jamii katika
nyanja zote muhimu akitaja afya,elimu na hata suala la uchumi.

Kwa upande wake KKKT imejipambanua kwa vitendo kwa kujenga hospitali kama ile ya Bumbuli wilayani Lushoto, Kilindi huku wakitoa michango Zahanati ya Mtimbwani jinni Tanga na Pwani.

Vilevile KKKT imekuwa na mchango mkubwa kwenye sekta ya elimu ambapo imediriki kubeba jukumu la kuwalipia ada wanafunzi na kwamba wanayo kamati inayohusika kusaidia wasiojiweza kama wazee.

Akizungumzia janga la UVIKO 19,alisema kwamba wameendelea kutoa elimu kwa waumini,kuchukua tahadhari na kuwakumbusha umuhimu wa kupata chanjo ya ugonjwa huo.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment