Friday, 24 February 2023

ZIARA YA MKUU WA MKOA WA TANGA,MGUMBA ILIKUWA HIVI KUTEMBELEA VIWANDA,,,,



Pichani mkono wa kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba katika ziara yake ya kutembelea viwanda akimshauri kitu Mkurugenzi wa kiwanda cha Vocha,Rashid Liemba (mkono wa kulia) kilichopo Gofu jijini.  

UONGOZI wa Kiwanda cha kuchakata kamba za Mkonge cha Pongwe (Pongwe Spinning Mill) kimeiomba serikali kuzuia uingizaji wa kamba bandia za nailoni ili kulinda soko la kiwanda hicho,.

Meneja  wa Kiwanda cha Kamba kilicho Pongwe halmashauri ya jiji la Tanga,,  Robert Semwaiko ambapo alimweleza Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omar Mgumba aliyetembelea kiwanda hicho jana kwamba kiwanda kimehujumiwa sana kutokana na kusambaa bidhaa hizo za kamba za nailoni katika masoko. 

Kiwanda hicho cha kamba za mkonge cha Pongwe kilicho njie kidogo ya jiji la Tanga kinapata hasara  katika uzalishaji kibiashara kutokana na ushindani na bidhaa za kamba za nailoni ambazo  huuzwa kwa bei ya chini sana ukilinganisha na bei ya kamba za mkonge, 

Semwaiki alisema awali kiwanda kilikuwa na wafanyakazi wapatao 300, lakini sasa hivi kina wafanyakazi 160 tu baada ya uongozi kulazimika kupunguza idadi kutokana na kuanguka soko la bei hiyo.

,Sisi tunauza kilo moja ya kamba ya mkonge kwa shilingin 5,000/- wakati kamba za nailoni zinauzwa kwa shilingi 3,000/-.” kwa kilo, Alisema Semwaiko na kuongeza kuwa huenda kiwanda kitapunguza wafanuyakazi zaidi iwapo kamba hizo bandia zitaongezeka.

Akizungumza baada ya kutembelea  na kukagua kazi kiwandani hapo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omar Mgumba alisema ni sera ya serikali ya kuruhusu biashara huria ili kuleta changamoto , lakini wakati huo huo kusimamia miongozo ya ufanyaji biashara ikiwa ni pamoja na ulipaji kodi.

Mkuu wa Mkoa aliahidi  kufuatilia suala la kamba bandia akisisitiza kuwa ufumbuzi utapatikana muda sio mrefu.

“Nia ya serikali ni kuona wafanyabiashara wanafanya shughuli zao kwa weledi na uaminifu bila kusahau ulipaji kodi stahiki”, alisema Mkuu huyo wa Mkoa.

Mwisho.




Mkuu wa mkoa wa Tanga katikati akikagua baadhi ya vocha kiwandani hapo,

Miongoni mwa viwanda cha Ashers kilipo gofu jijini Tanga.

 

No comments:

Post a Comment