Tuesday 30 April 2024

MAHAFALI YA 64 CHUO CHA UALIM KOROGWE MKOANI TANGA YALIKUWA HIVI 2024,

Pichani ni miongoni mwa wahitimu wa chuo cha ualim Korogwe siku ya mahafali.

NA SOPHIA WAKATI,KOROGWE
SERIKALI ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt.  Samia Suluhu Hassan imetoa mikopo zaidi ya Shilingi million 40 za kitanzania  kwa wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Korogwe, Mkuu wa Chuo hicho cha, Hassan Abdillah Ismail ameeleza.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa chuo cha Ualimu Korogwe,Abdilah Ismail ametoa taarifa hiyo wakati akizungumza kwenye mahafali ya Wahitimu 259 wa stashahada ya Ualimu ambapo alisema fedha hizo tayari zimeshakabidhiwa kwa wanafunzi husika.

Ismail amewasilisha shukrani zake kwa Serikali kutokana na hatua yake hiyo ya kuwezesha mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya ualimu na vile vya kati jambo ambalo hapo awali halikuwahi kuwepo.

Aidha Mkuu huyo wa chuo cha ualimu alisema, mitihani kwa wahitimu hao wote inatarajiwa kuanza Mei 6 mwaka huu huku wanafunzi hao wakiwa wamesoma masomo ya Sayansi ili kuwa walimu wa sekondari na kwamba wameandaliwa vizuri kitaaluma na kimaadili.

Kwa uoande wake Kaimu afisa elimu idara ya elimu Sekondari katika Halmashauri ya Mji Korogwe, Omari Mlawa aliwashauri wahitimu hao kwenda kujishughulisha na kilimo na ujasiriamali wakati wakisubiri ajira zao.

Alisema,licha ya kufahamika uwepo wa changamoto ya ajira,wahitimu hao hawapaswi kusubiri ajira badala yake wakajikite kwenye kilimo na ujasiriamali ili kuweza kujikwamua kiuchumi.

Pamoja na hayo, Mlawa alisema kwamba Halmashauri ya Mji Korogwe imejipanga kuwatumia wahitimu hao katika shule zilizopo kwa mtindo wa kujitolea huku wakiwalipa kiasi kidogo cha fedha za Sabuni. 

Aidha,aliwashauri wahitimu hao kutokusita kuwasilisha barua zao za maombi ya ajira za kujitolea kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe ili kuweza kupata fursa hiyo ya kufundisha.

Katika risala ya wahitimu wa Stashahada ya Ualimu iliyosimwa na Sharon Faustin Shaigwa alisema, chuo kinakabiliwa na changamoto udogo wa maabara ya Tehama ikilinganishwa na idadi kubwa ya wanafunzi.

Changamoto nyingine ni uchakavu wa miundombinu ya maji taka,kukosa uzio,ukosefu wa daktari, uhaba wa samani na upungufu wa vifaa tiba.
Mwisho.


Wahitimu.

Pichani ni Rais wa wanafunzi chuo hicho,Sharon Faustin ni miongoni mwa  wahitimu wanaomaliza masomo yao huku akishiriki Mahafali ya 64 kwa niaba ya wenzake ameahidi kwenda kuitumia vyema taaluma waliyopata na kwamba watafanya kazi kwa bidii kupitia nyanja mbalimbali ikiwa sehemu ya mafunzo waliyoyapata chuo cha ualimu Korogwe.


Pichani ni miongoni mwa wahitimu ,Husna  Benjamin amesema ataenda kutumia taaluma yake kwenda kuelimisha jamii na watu waamini hakuna kitu kigumu katika maisha na kuiomba serikal kutoa ajira.

Wahitimu wa chuo hicho.





 

No comments:

Post a Comment