Sunday 22 October 2017

TAASISI YA WICOF YA MKOANI MOROGORO IKIWA KATIKA ZOEZI LA KUGAWA MISAADA MKOANI TANGA,,,,

Pichani mkono wa kushoto mwanamke ambaye amevaa baibui jeusi ni mwanachama wa  taasisi ya WICOF,Zainab Bendera akifuatiwa na Mohamedi Dhahabu wakikakabidhidhi misaada kwa watumishi wa hospital ya rufaa Bombo mkoani Tanga,
 Pichani wa pili mkono wa kushoto ni mwenyekiti wa taasisi ya WICOF, Mwajabu Dhahabu mwanachama wake Zainab Bendera juzi katika ziara ya kugawa misaada husika ilisambazwa hospitali yarufaa Bombo Jijini Tanga na Zahanati ya Potwe iliyopo wilayani Muheza katika mkoani hapo.
Pichani ambaye amevaa baibui ni mwanachama wa WICOF,Zainab Bendera juzi katika zoezi la kugawa misaada husika ilisambazwa hospitali yarufaa Bombo Jijini Tanga na Zahanati ya Potwe iliyopo wilayani Muheza katika mkoani hapo.
Ugawaji wa madawa Zahanati ya Potwe iliyopo wilayani Muheza katika mkoani Tanga ilikuwa hivi.
Picha ni wananchi mara baada kukabidhiwa msaada wa madawa kwa ajili ya Zahanati ya Potwe iliyopo wilayani Muheza katika mkoani Tanga wakiwa kwenye picha ya pamoja.


 Picha ni vifaa mbalimbali vya msaada vilivyotolewa na taasisi ya WICOF yenye maskani yake mkoani Morogoro,kwa ajili ya kuhifadhia maziwa kwa ajili ya watoto.


NA SOPHIA WAKATI, TANGA
TAASISI ya Wanawake Women Infants and Community Outreach Foundation (WICOF) imetoa msaada wenye thamani ya zaidi sh 3.1 million kusaidia Wagonjwa kwenye baadhi ya hospitali na Zahanati katika mkoa wa Tanga. 

Mwenyekiti wa taasisi hiyo Mwajabu Dhahabu amesema juzi kuwa misaada husika ilisambazwa hospitali yarufaa Bombo Jijini Tanga na Zahanati ya Potwe iliyopo wilayani Muheza katika mkoani hapo. 

Dhahabu ametaja misaada hiyo kuwa ni shuka 36 kwenye Wodi ya watoto Bombo hospitali, deep freezer la kuhifadhia maziwa ya watoto pamoja na dawa mbalimbali pamoja na vifaa tiba. 

Alifafanua kuwa maeneo yote hayo misaada waliyoitoa imegharimu zaidi ya sh 3.1 milioni ikiwa ni sehemu ya mchango wao katika kusaidia huduma za afya kwa jamii. 

Naye mwanachama wa asasi hiyo ya WICOF yenye makao yake makuu mjini Morogoro, Zainab Bendera alisema wamejipanga kusaidia huduma za jamii hasa sekta ya afya ili kuokoa nguvu kazi. 

Alisema, tayari wamechukua michoro inayoihusu Zahanati ya Potwe ili kuangalia namna watakavyoweza kushiriki kuifanyia ukarabati na hivyo kutoa huduma zenye ubora na viwango stahiki. 

"Tukiwa sehemu ya watanzania tumeguswa kuisaidia jamii yetu, tunaunga mkono jitihada za Serikali yetu kupitia kauli mbiu ya hapa kazi tu "alisema Bendera. 

Aidha Bendera ametoa wito kwa asasi nyingine wakiwemo mtu mmoja mmoja wenye uwezo kujitokeza kusaidia sekta ya afya ili kuweza kuimarika na kuleta tija kwa watanzania walio wengi.
Mwisho. 

No comments:

Post a Comment