Wednesday 22 November 2017

VIFAHAMU VIKOSI VINNE VYA FAIR PLAY IKIWEMO YA WANAWAKE AMBAO WANAJIWENDA NA LIGI KUU YA TAIFA,,

 TIMU ya Soka la Wanawake Fair Play Queens ya Jijini Tanga inaendelea na mazoezi yake katika viwanja vya Disouza lengo likiwa kufanya maandalizi kabambe kujiandaa na Ligi ya Taifa.
Kikosi hicho cha Fair Play Queens kinatarajiwa kuondoka Jijini Tanga kuelekea Jijini Dar es salaam mahali ambapo Premier League inafanyika.

Msemaji wa kikosi cha Fair Play Queens, Sophia Wakati amesema maandalizi yanakwenda vyema licha ya changamoto ndogondogo kujitokeza.

"Tunaendelea na mazoezi makali chini ya kocha wetu Idd Kuha na kwa jinsi anavyowanoa wachezaji niseme tu hali sio mbaya, tunaamini tutafanya vizuri "alisema Sophia Wakati msemaji wa kikosi cha timu ya Fair Play Queens.

Hata hivyo msemaji huyo wa kikosi cha Fair Play Queens alitoa wito kwa wadau wa mchezo wa Soka kujitokeza kwa wingi kufadhili timu zinazowahusu Wanawake kutokana na mwamko wa wananchi kuzisaidia kuwa mdogo. 

Amesema, kitendo cha wadau kujitokeza kufadhili mchezo huo kwa kada ya Wanawake kutaamsha ari ya wachezaji kufanya vyema jambo ambalo pia litaibua ajira kwa jinsia hiyo.
Ligi hiyo ya Taifa Wanawake inatarajia kuanza kutimua vumbi hapo Nov 27 mwaka huu ambapo awali itakuwa katika mtindo wa makundi miwili. 

Kwa mujibu wa habari kutoka kwa msemaji huyo wa Fair Play Queen katika kundi lao litakaokipiga Jijini kuna timu za Simba Queen, JKT, Mlandizi, Mburahati na Ever Green na kituo kingine kunakuwepo huko Jijini Arusha. 

Kapteni msaidizi wa timu ya Fair Play,Cristina Fransis 'Kazola' juzi uwanja katika mahojiano na Mwandishi wa makala haya amejinasibu kwamba kikosi chake kiko imara kuivaa Simba Queen katika mchezo wa ufunguzi. 

Kazola amesema, kwa mazoezi waliyoyapata kupitia mwalimu wao Kuha ni dhahiri kwamba wamepata mbinu za ziada kuwasambaratisha wapinzania wao hao Simba Queens kwenye mchezo wa ufunguzi hivyo kujiweka vyema. 

Amesema,kwa mwaka huu wamejipanga kuibuka mabingwa wa ligi hiyo ingawa alisema kupata ushindani kutoka kwa wapinzania wao itakuwa jambo la kawaida kwa vile hakuna atakayekubali kupoteza mchezo kirahisi. 

"Ushindani tunaamini ya kuwa utakuwepo ila kwetu sisi hatuendi kutembea inahitaji bingwa tukianza kuusaka katika mchezo wetu wa ufunguzi "alisema Kazola. 

Katika taarifa yake kwa gazeti hili meneja wa Fair Play Queen Khalid Abdallah alisema kikosi chake kitaondoka Jijini Tanga wakati wowote kuanzia sasa (23/11/2017)ili kuweka kambi ya mazoezi kuzoea mazingira huko Jijini Dar es salaam. 

Alisema, viongozi watakaoambatana na timu hiyo licha ya wachezaji wote ni mwalimu Idd Kuha, datari wa timu, kocha msaidizi na
Mwisho.

 Pichani mkono wa kushoto amesimama ni mkurugenzi wa vikosi hivyo ambaye ni mchezaji wa zamani wa timu ya Coastal Union ,Khald Abdallah juzi mara baada ya mazoezi akiwapa maelekezo na mbinu mbalimbali za mchezo huo uwanja wa soka D'Souza jijini Tanga.



 Pichani mkono wa kushoto amesimama ni mkurugenzi wa vikosi hivyo ambaye ni mchezaji wa zamani wa timu ya Coastal Union,Khald Abdallah akiwapa maelekezo na mbinu mbalimbali za mchezo huo uwanja wa soka D'Souza jijini Tanga.

No comments:

Post a Comment