Wednesday 22 November 2017

ZIARA YA WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKAL ZA MITAA,JAFFO MKOANI TANGA ILIKUWA HIVI,,

Pichani ni 'WAZIRI wa Nchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,Suleiman Jaffo ameziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa hadi kufikia mwaka ujao zinalipa asilimia kumi (10%) za vijana na wanawake ili kuziwezesha kujikwamua kiuchumi.


Waziri Jaffo alitoa agizo hilo jana alipokuwa akipokea taarifa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tanga kwa ziara ya kikazi akisema kuwa ulipaji wa fedha hizo za vijana na wanawake ni agizo la serikali kupitia chama tawala akisistiza kusema kuwa tayari fedha hizo zilishatengwa kwa kada hiyo.

Alisema katika agizo hilo utekelezwaji wake umekuwa mdogo ambapo mpaka sasa kuna baadhi ya halmashauri bado hazijatekeleza adhima hiyo  ikiwa ni moja ya mkakati wa serikal na ilani ya chama cha mapinduzi. 

Akionyesha msisitizo juu ya fedha hizo za vijana na wanawake,Waziri Jaffo alisema kuwa iwapo wahusika watapatiwa stahili hiyo itakuwa rahisi kwao kupata mitaji na hivyo kuendesha shughuli mbalimbali za kiuchumi na kuondokana na hali tegemezi hapa nchini.

“Viongozi fedha hizi zipo na tayari zilishatengwa na serikal,kila halmashauri imnapewa mil 61.5 hivyo kila halmashauri inatakiwa kuhakikisha kwamba hadi kufikia mwakani iwe imeshalipa asilimia kumi (10%) ya fedha za wanawake na vijana”alisema Waziri huyo Suleiman Jaffo.

Aidha,Pia ameliagiza Jiji la Tanga kuhakikisha kwamba inawatengea eneo maalum mafundi cherahani ili kuweza kuendesha shughuli zao kwa tija ambapo alisema kuwa kwa kufanya hivyo itasaidia kukuza ajira miongoni mwa jamii hasa kada ya vijana.

Mbali na hayo katika mazungumzo yake wakati akipokea taarifa ya mkuu wa wilaya ya Tanga,Waziri Jaffo alitumia fursa hiyo kuwataka watumishi kuendelea kuchapa kazi kwa kujituma hatua aliyoieleza kuwa itasaidia kuiwezesha serikali kufikia malengo yake.

Awali mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa katika taarifa yake alimweleza Waziri Jaffo kuwa Tanga imetenga maeneo ya viwanda huko Kiomoni ekari 101 na Mabokweni ekari 117 hatua ambayo ilipongezwa na Waziri huyo wa Tamisemi.

Katika pongezi zake hizo Waziri Jaffo alisema amefurahishwa na hatua hiyo ya Tanga kuunga mkono agizo la serikal kutenga maeneo huku akitanabaisha kuwa kimkakati Tanga ni miongoni mwa mikoa ya viwanda ambapo kunahitajika uwepo wa viwanda vidogo na vile vya kati ili kukuza uchumi.

Naye mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga,Dudi Mayeji alieleza kuwa wamefanikiwa kufanya marekebisho kwenye barabara zake na hivyo kuwezesha miundombinu hiyo kuwa kwenye ubora na kulifanya Jiji kurejea hadhi yake .

Katika ziara hiyo baadhi ya maeneo ambayo ametembelea Waziri huyo wa ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa ni kituo cha Televisheni ya jamii TaTv,eneo la Pongwe kwenye shule yenye watoto wenye mahitaji maalum,shule ya msingi Kiomoni kuweka jiwe la msingi,shule ya msingi Bombo kukagua maendeleo ya ujenzi na kukagua dula la dawa la jamii.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment