Wednesday 22 November 2017

WADAU WA UTALII WATAKIWA KUITANGAZA HIFADHI YA NILO WILAYANI KOROGWE,,

Pichani ni Mhifadhi mkuu wa Nilo,Fabian Mukome juzi akizungumzia lengo la kuandaa Washa hiyo ni kuwakutanisha Wadau wa sekta ya utalii ili kuwapatia uelewa juu ya vivutio vya utalii vinavyo patikana kwenye hifadhi hiyo ya Nilo iliyopo Wilayani Korogwe mkoani Tanga.

NA SOPHIA WAKATI,TANGA.
WADAU wa sekta ya Utalii wametakiwa kuhakikisha kuwa wanakuwa mabalozi wazuri wa mhifadhi mkuu wa Nilo,Fabian Mukome amesema lengo la kuandaa Washa hiyo ni kuwakutanisha Wadau wa sekta ya utalii ili kuwapatia uelewa juu ya vivutio vya utalii vinavyo patikana kwenye hifadhi hiyo ya Nilo iliyopo Wilayani Korogwe mkoani Tanga.

Afisa wa Maliasili Mkoani Tanga, Timothio Sosiya ametoa rai hiyo juzi wakati akifunga washa ya siku mbili ya wadau yenye lengo la kuwajengea uelewewa juu ya vivutio vya utalii ndani ya hifadhi ya Mazingira ya Nilo iliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha ufundi veta Jijini Tanga.

Warsha hiyo ilihudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka mikoa ya Arusha, Manyara, Moshi na Tanga ambapo alisema kuwa waongozaji watalii,wamiliki wa Hoteli na chama cha Waandishi wa Habari za mazingira TARUJA wanayo nafasi kumbwa ya kutangaza vivutio vinavyopatikana katika hifadhi hiyo.

"Wakati umefika sasa kwa wadau kila mmoja wetu kuchukua nafasi yake kutangaza vivutio vya utalii kwenye maeneo yetu,aidha hii hifadhi ya Nilo tusaidiane kuitangaza"alisema Ofisa huyo wa maliasili  mkoani hapo Sosiya.

Kwa upande wake mhifadhi mkuu wa Nilo,Fabian Mukome amesema lengo la kuandaa Washa hiyo ni kuwakutanisha Wadau wa sekta ya utalii ili kuwapatia uelewa juu ya vivutio vya utalii vinavyo patikana kwenye hifadhi hiyo ya Nilo iliyopo Wilayani Korogwe mkoani Tanga.

Miongoni mwa wadau walioshiriki Warsha hiyo,Nelvine Peter kutoka Gladys Safari mkoani Moshi amepongeza jitihada zilizoanzishwa kuwaongezea uelewa juu ya umuhimu wa kuitangaza vivutio vya utalii kwenye maeneo yao kuleta tija kwa jamii mzima.

Agnes Mkala kutoka Panama Gaden hotel mkoani Moshi alisema kuwa kupitia Warsha kama hizo zimeweza kuwasaidia kubainika mambo mengi ambayo awali wakikosa kuyafahamu ambapo sasa watachukua hatua kuvitangaza vivutio vilivyopo.

Aidha Wadau hao wakati wa kuhitimisha Washa yao wametembelea kwenye hifadhi hiyo ya Nilo iliyopo wilayani Korogwe ili kuangalia vivutio mbalimbali ikiwemo maua na Vinyonga wenye mapembe ambao wanapatikana kwenye hifadhi hayo pekee hatua itakayosaidia kuutangaza utalii na kukuza uchumi.
Mwisho

No comments:

Post a Comment