Thursday 21 December 2017

KAMANDA MPYA WA JESHI LA POLISI MKOA WA TANGA,,BUKOMBE AMEWATAKA WAMILIKI WA KUMBI ZA STAREHE KUHAKIKISHA WANAFUATA SHERIA ILIYOPO ILI KUEPUKA KUMBUGHUZI MTU,,,

 Pichani ni Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga Kamishna msaidizi mwandamizi,Edward Bukombe Selestin akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake (hawapo pichani) na kujitambulisaha ambapo amesema kuelekea kumaliza mwaka 2017,hali ya uhalifu mkoani hapo ni amani na utulivu huku akibainisha mkakati uliopo kudhibiti vitendo vya uhali katika kusheherekea sikukuu ya krismasi na mwaka mpya.

NA SOPHIA WAKATI, TANGA
KATIKA kusherehekea Sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya, jeshi la Polisi Mkoani Tanga limewataka Wamiliki wa kumbi za starehe kuzingatia sheria iliyopo ili kuepuka kubugudhi watu wengine.

Licha ya kutoa rai hiyo kwa wamiliki kumbi za starehe pia jeshi hilo limewataka wananchi kujiepusha na vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani kama milipuko ya baruti na fatalities.

Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga Kamishna msaidizi mwandamizi,Edward Bukombe Selestin ametoa wito huo LEO wakati akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake na kujitambulisaha na kueleza kuhusiana na hali ya ulinzi na Usalama kuelekea kumaliza mwaka.

Akizungumzia kumbi za starehe Kamanda,Selestin alisema, wamiliki mkoani hapo wanapaswa kuzingatia sheria inayodhibiti mtu kufanya shughuli zake bila bugudha kwa wengine.

Aidha Kamanda huyo alisema, sheria ya kumbi za starehe za Usiku 'Night Club'ziko wazi zikielekeza shughuli zote kufanyika ndani huku alitanabaisha kuwa Bar na sehemu nyingine Mwisho wao unatakiwa kuwa saa tano usiku.

Kuhusu milipuko, alisema kuwa mtu kujihusisha na vitendo hivyo ni kinyume cha sheria namba 13 ambapo adhabu yake ni faini shilingi milioni tano, kifungo miaka mitatu au vyote viwili kwa pamoja.

Kamanda Selestin alitumia fursa hiyo kutoa msisitizo kwa maeneo ya nyumba za Ibada akiwataka viongozi wake kuhakikisha wanaendesha Ibada kwa muda muafaka ili kuepuka mkanganyiko.

Kamanda huyo wa jeshi la Polisi Mkoani Tanga Kamishna msaidizi mwandamizi,Selestin amebainisha kuwa kipindi cha kuanzia mwenzi January hadi Novemba 2017 jumla ya matukio ya uhalifu 16799 yameripotiwa tofauti na mwaka jana 17548.

 Pia amebainisha kwamba jeshi la polisi katika kipindi hicho limefanikiwa kuendesha misako na operesheni katika maeneo mbalimbali na kufanikiwa kukamata wahalifu na vielelezo vya kesi ikiwemo bhangi yenye uzito wa kilogramu 761.1,huku kesi 37 zimefunguliwa.

Huku mirungi yenye uzito wa kilogramu 5396,740 zilikamatwa,madawa ya kulevya ya viwandani jumla ya kesi 55 zimefunguliwa baada ya uzito wa kilogramu 3.749 kukamatwa.

Kwa upande wa kudhibiti wahamiaji haramu 224 walikatwa kipindi hicho cha January hadi Novemba 2017 huku wasomali wakiwa 55,waEthiopia 149 na raia wa nchi jirani wa Kenya wakiwa 20.

Kamanda, Selestin ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa jamii kuendelea kushirikiana na jeshi hilo kupeana taarifa hatua ambayo itachangia kudhibiti vitendo vya uhalifu katika mkoa mzima wa Tanga.

"Kiukweli kipindi hiki cha kuelekea msimu huu wa sherehe za sikukuu za krismasi na mwaka mpya jeshi la polisi limejipanga kuimarisha hali ya ulinzi na Usalama wakati wote huo"alisema kamanda Selestin.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment