NA SOPHIA WAKATI,TANGA
KAMPUNI
ya Katani Limited yenye
makao makuu yake Jijini Tanga, imesema ina mpango wa kuwa miongoni mwa
wadhamini wa klabu ya Coastal Union ili kuweza kufanya vizuri michuano
ya ligi kuu msimu ujao Tanzania bara.
Hata hivyo,imesema kadiri itakavyokuwa na uzalishaji
wa kiwango cha juu katika malighafi inayotokana na zao la Mkonge,itaidhamini moja kwa moja klabu hiyo ya Coastal Union
inayoshiriki Ligi ya Vodacom.
Akizungumza na Waandishi wa
Habari ofisini kwake jana,mara baada ya kutangaza kuingia udhamini wa mashindano ya
'Tanga City Marathon 2018',Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo,Juma Shamte,.
Alisema
kuwa lengo la kujiingiza kwenye michezo ni njia
mojawapo ya kuhamasisha ulimaji wa zao la mkonge kwa wakulima na
wanunuzi wa bidhaa inayotokana na zao hilo ndani na nje ya nchi.
Alibainisha kuwa kadiri watakavyoweza
kukua na kuzalisha kwa wingi bidhaa zitokanazo na mkonge, wataweza kuwa
na fursa zaidi ya kujiingiza katika michezo na kwamba wanaweza kukutana
na viongozi wa Coastal wakatazama kama wanaweza
na wao kuifadhili.
"Kiukweli kadiri tunavyokuwa na kuzalisha
tutaweza kutoa fursa zaidi za kujiingiza katika michezo ni suala la
kufanyia kazi kama tunaweza, kukutana na viongozi wa Coastal kuangalia ni jinsi gani tunaweza kushiriki " alisema Shamte.
Shamte alisema kampuni hiyo
ambayo ina mashidnano yake ya endelevu kila mwaka yanayofahamika kwa
jina la 'Mkonge Cup' kwa kushirikisha timu mbalimbali za madaraja ya
chini.
Hata hivyo,kampuni hiyo imekabidhi hundi ya
shilingi milioni 7 kwa waandaaji wa mashindano hayo ambayo yatafanyika
Machi 31 na jumla ya washiriki 500 hadi sa sa wamejiandikisha kushiriki
mbio hizo.
Alisema aliongeza kuwa kadiri watakavyoweza
kukua na kuzalisha kwa wingi bidhaa zitokanazo na mkonge, wataweza kuwa
na fursa zaidi ya kujiingiza katika michezo na kwamba wanaweza kukutana
na viongozi wa Coastal wakatazama kama wanaweza
na wao kuifadhili.
"Kiukweli
kadiri tunavyokuwa na kuzalisha
mzuri tutaweza kutumia fursa zaidi za kujiingiza katika michezo,kwa
kukutana na viongozi wa Coastal ili kuangalia tunashiriki vipi,"
alisema.
Shamte
alisema kuwa lengo kubwa ni kusaidia timu mbalimbali za madaraja ya
chini ili kuweza kuibua vipaji na kujitangaza kupitia sekta hiyo ya
michezo.
Hata hivyo,kampuni hiyo imekabidhi hundi ya
shilingi milioni 7 kwa waandaaji wa mashindano hayo ambayo yatafanyika
Machi 31 na jumla ya washiriki 500 hadi sasa tayari wamethibitisha kushiriki
mbio hizo.
No comments:
Post a Comment