Sunday 18 March 2018

BAADA YA TIMU YA COASTAL UNION KUPANDA DARAJA,,

 Pichani ni mwenyekiti wa Klab ya Coastal Union,Steven Mnguto akizungumzia mkakati uliopo katika kujiandaa na ligi kuu tanzania bara.
 Pichani ni mwenyekiti wa chama cha mpira mkoa wa Tanga,Said Soud akizungumzia furaha yake kwa timu hiyo kupanda daraja,
 Pichanikatikati mwanamke ni  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalim mara baada ya kukabidhi eneo la michezo kwa uongozi wa timu ya Coastal Union kama furaha yake baada ya timu hiyo kupanda daraja,akiwa na viongozi na baadhi ya wanachama wa timu hiyo.

 Pichanikatikati mwanamke ni  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalim mara baada ya kukabidhi eneo la michezo kwa uongozi wa timu ya Coastal Union kama furaha yake baada ya timu hiyo kupanda daraja.

Pichanikatikati mwanamke ni  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalim mara baada ya kukabidhi eneo la michezo kwa uongozi wa timu ya Coastal Union kama furaha yake baada ya timu hiyo kupanda daraja.



NA SOPHIA WAKATI,TANGA
UONGOZI klabu ya Coastal Union yenye maskani yake barabara ya 11 Jijini Tanga imesema itamuunga mkono na kuwa naye bega kwa bega Mbunge wa Viti maalum  Mkoani Tanga, Ummy Mwalimu katika harakati zake zote za kuwaletea Maendeleo wananchi wa Tanga. 

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa mpito wa klabu hiyo,Stephen Mnguto wakati akishukuru kwa kukabidhiwa eneo ambalo watakalojenga uwanja wa mpira wa klabu hiyo.

 Alisema kuwa Kitendo alichofanya mbunge hyo Ummy kuwapa eneo watakalojenga uwanja ni jambo kubwa lililoandika historia ya klabu hiyo tangu ianzishwe Mwaka 1948.

"Kiukweli mheshimiwa hili ulilotufanyia umetujengea heshima kubwa kwa klabu yetu na sisi kulipa fadhila tunakuahidi tutakuunga mkono kwa jambo lolote la maendeleo utakalolifanya lenye maslahi kwa watu wa Tanga, "alisema Mnguto. 

Eneo hilo lililopo mtaa wa Kichangani kata ya Maweni Jijini hapa linaukubwa wa mita za mraba zipatazo 7,632 yenye thamani ya sh. 38,160,000 ambalo limetolewa na mbunge huyo kwa kushirikiana na kampuni ya City Plan ya Jijini Dar es salaam. 

Mkurugenzi wa kampuni ya City Plan Dk. Juma Mohamed alisema eneo hilo wamelitoa kwa klabu hiyo baada ya kuombwa na Ummy kwa ajili ya kujengwa uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu wa Coastal. 

Hata hivyo, Dk. Mohammed alisema baada ya kutenga eneo, waliacha wazi eneo jingine lililipo jirani na kiwanja hicho lenye ukubwa wa mita za mraba zipatazo 9,0000 zenye thamani ya sh. 48,000,000 kwa ajili ya kujengwa hosteli za wachezaji wa timu hiyo vyumba vya kufanyia mazoezi ya viungo.

Kuzungumza katika hafla hiyo fupi iliyofanyikia eneo la uwanja huo na kuhudhuriwa na mashabiki kadhaa kikiwemo kikundi cha ngoma cha timu hiyo, Ummy ambaye pia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, alisema amekabidhi kiwanja hicho kama furaha yake baada ya timu hiyo kupanda daraja.

Aidha,alisema baada ya timu kupanda daraja pia aliahidi kuiletea maendeleo ili timu hiyo iweze kushiriki Ligi Kuu kwa mafanikio na kuiletea heshima mkoa wa Tanga kupitia michezo.

"Nawapongeza sana City Plan kwa kuunga mkono jitihada zetu za kuindeleza Coastal Union, kilichobaki tuzidi kushikamana ili tuweze kufanya vizuri zaidi, "Alisema Ummy. 

Waziri huyo aliahidi kutafuta fedha nyingine kiasi cha Shilingi milioni 48 ili aweze kuchukua eneo jingine lenye viwanja 16 kwa ajili ya kujengwa hosteli ya klabu hiyo kongwe hapa nchini. 

Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa alimpongeza Waziri Ummy kwa jitihada zake za kuisaidia timu hiyo ambayo kupanda kwake daraja kulitokana na jitihada zake za kurudisha umoja uliokosekana kwa klabu hiyo hapo awali.

Nae Mwenyekiti wa chama cha soka Mkoani Tanga  (TRFA)  Said Suod alimpongeza Waziri Ummy kwa hatua ya kufanikisha kupatikana uwanja huo kwa klabu hiyo baada ya kutimiza miaka 70 tangu  kuanzishwa kwake lakini haukuwa na uwanja wake.
Mwisho.





No comments:

Post a Comment