Timu ya soka ya Shirika la umeme Pemba Zanzibar ZECO mara baada ya mechi katika ziara yao mkoani Tanga.
NA SOPHIA WAKATI,TANGA
TIMU ya soka ya Shirika la Umeme
Tanesco mkoani Tanga juzi imetoka kifua mbele baada ya kuifunga Shirika la umeme
Pemba Zanzibar ZECO kwa magoli 3-1.
Baada ya kuingia kwa magoli hayo kipindi
cha pili cha mchezo huo Tanesco Pemba ilikuja ilijipanga kuonyesha kandanda ambayo yalileta mafanikio dakika ya
63 ilifanikiwa kusawadhisha goli moja kupitia Salehe Abdallah Kassim..
Katika mchezo wao wa kwanza kwenye ziara yao
hiyo mkoani Tanga, ZECO waliwachapa Worrier
ya jijini hapo kwa magoli 2 kwa 1,.
Magoli ya ZECO katika mchezo wake dhidi ya
Worrier yalifungwa na vinara wa timu hiyo Omari Ramadhani Fadhil na Jamil Issa Ally dakika ya 27 na 41.
Afisa uhusiano wa shirika la umeme tawi la Pemba
ZECO,Amos Salum
Masoudi alisema,lengo la ziara yao ni kujenga
uhusiano hatua ambayo
husaidia kuleta ufanisi kazini.
Naye kiongozi wa kikosi cha Tanesco Tanga, Muhsin Mselemu alisema kwamba mchezo huo wa ujirani mwema ni muhimu utasaidia kuboresha mahusiano kazini na kujenga undugu eneo la kazi.
Mwisho.
Ni jambo jema kwa Tanesco kucheza na Jirani zao wa zeco kwani itasaidia kuongeaza uhusiano mwema na ufanisi katika kazi
ReplyDelete