Monday, 10 October 2022

KAMPUNI YA AGRICOM IMESEMA KUWEKA KAMBI JIJINI TANGA IMEFANIKIWA KUZINDUA KAMPENI YA MTUMISHI SHAMBANI, ILI KURAHISISHA KUTIMIZA NDOTO ZAO ZA KILIMO,,,

Pichani ni Afisa masoko wa kampuni  ya Agricom Afrika,Baraka Konkara akieleza lengo la kuwekeza kambi kwenye sekta ya michezo kupitia SHIMIWI ni kuwasaidia watumishi kujishughulisha na  kilimo.

NA SOPHIA WAKATI,TANGA

KAMPUNI ya Agricom Afrika imesema ina mpango mkakati wa  kuwekeza kwa wakulima wa zao la mkonge nchini ili kuwawezesha kulima zao hilo kwa tija na kuinua  kipato na uchumi wao kwa kulima kisasa.

Kauli hiyo imetolewa leo na Afisa Masoko wa Kampuni hiyo, Baraka Konkara ambapo amesema kwamba lengo la kuwekeza katika zao hilo ni kutoa fursa kwa wakulima wa mazao mbalimbali ili waweze kunufaika na fursa zilizopo.

Alisema tayari wameshajenga mahusiano mazuri baina yao na wakulima wa zao  la mkonge ikiwemo Amcos mkoani Tanga lengo likiwa ni kulima kilimo cha kisasa na kuwawezesha kunufaika na kilimo

“Kiukweli kuna haja kubwa ya wakulima kuweza kubadilika kulima kisasa ,kuleta tija kupata mavuno  yenye kuleta mafanikio kwa mtumishi,hivyo ni  muhimu kutumia zana za kisasa kutoka kwenye kilimo cha mazoea,”alisema Afisa masoko huyo Konkara huku akisistiza wakulima  kujitokeza kunufaika na kampuni hiyo.

Konkara alibainisha kwamba lengo la kampuni hiyo kuwekeza ni baada ya kuona ndani ya miaka mitatu zao hilo kuonesha kuleta mabadailiko  katika faida zake hapa nchini.

Akizungumzia zaidi afisa masoko huyo alisema kuwa tangu kuwekeza kwenye michezo jijini Tanga kujikita kutoa elimu kwa watumishi   na jamii,tumeweza kuona mabadiliko na mwamko   mkubwa kwa baadhi wananchi wa kada mbalimbali kujitokeza  kuhitaji  huduma za mikopo vifaa vya kilimo.

Hata hivyo,alisema kwamba lengo la kuweka kambi kuitumia michezo ya SHIMIWI   ili kuisaidia serikali ya Awamu ya sita kupitia sekta ya michezo na kilimo kutengeneza mazingira rahisi zaidi watumishi kujiongezea kipato kupitia shambani.

Pia alitumia nafasi hiyo  kuiomba serikali kutengeneza mazingira mazuri kwa  Wizara , idara na Taasisi za serikali ili waweze kukopa au kununua vitendea kazi  ili kutimiza lengo la mtumishi Shambani.

Afisa masoko huyo, alizitaja miongoni mwa AMCOS ambazo tayari wameshafanya mazungumzo ili kuziwezesha kuwapata wakulima wa zao la Mkonge ni Magunga , Mwerya ,Magoma, Hale zilizopo Korogwe Mkoani Tanga.

Pia alibainisha kueleza kwamba tayari Agricom imefanikiwa kuketi na Bodi ya Mkonge Tanzania,lengo likiwa kuweka mazingira mazuri ya kuongeza tija kwa wakulima na kuwajengea uwezo kutimiza ndoto zao kupitia kilimo.

 Mwisho. 



Pichani ni Afisa masoko wa kampuni  ya Agricom Afrika,Baraka Konkara akiwa uwanja wa soka Mkwakwani akionyesha vitendea kazi ambavyo vimekuwa vikikopeshwa kwa watumishi kwa ajili ya kujikita na kilimo.

No comments:

Post a Comment