Tuesday, 8 November 2022

TAKUKURU MKOANI TANGA,IKIFAFANUA JINSI ILIVYOFANIKIWA KUBAINI WAGONJWA HEWA 313 WA VVU WILAYANI MUHEZA,,

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga ,Zainabu Bakari akitoa taarifa kwa waandashi wa habari jijini Tanga(hawapo pichani) katika uchunguzi ilivyofanikiwa kubaini wagonjwa hewa idara ya afya.

NA SOPHIA WAKATI,TANGA

TAASISI  ya kuzuia na Kupambana na rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Tanga ,katika uchunguzi imefanikiwa kubaini jumla wa wagonjwa hewa 313 wa VVU Kwenye mfumo wa Usajili wa wagonjwa hao wilayani Muheza kwa lengo ili kuonyesha takwimu ziko juu ili kujinufaisha.

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Tanga ,Zainabu Bakari wakati akitoa taarifa hiyo ofisini kwake wakati akizungumza na waandashi wa habari jijini Tanga.

Akisoma taarifa yake ya kipindi cha julai hadi September mwaka huu,alisema kwamba  awali TAKUKURU ilipata taarifa kutoka kwa wasamalia wema kwamba kuna baadhi ya watoa huduma idara za afya wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya kufanya udanganyifu wa kusajili watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi VVU kinyume na utaratibu.

 Alisema kuwa watoa huduma hao walikuwa wakiingiza majina hewa ya wagonjwa ili kuonyesha kuwa twakimuza za wanaoishi na VVU kuonekana ziko juu kwa maslahi yao binafsi huku ikiwa ni kosa kisheria.

Mkuu huyo wa TAKUKURU mkoani Tanga,Zainabu alisema  baada yakupokea na kufuatilia baadhi ya Zahanati wilayani Muheza,kuanza utekelezaji wa majukumu yao na kufanikiwa kubaini kuna wagonjwa 313 ambao siyo halisi  kwa upatikanaji wake.

''Takukutu baada ya kupata taarifa kufuatilia wahudumu wa afya wanaohusika na zoezi la kuwasajili na kuwafuatilia wagonjwa wanaoishi na VVU,pia tumebaini wamekuwa wakilipwa posho ya gharama ya usafiri shilingi 20,000 kwa siku kila wanapotoka kwenda kuwatembelea wagonjwa''Alisema Zainabu. 

 Mkuu huyo wa TAKUKURU mkoani Tanga,Zainabu alibaisha kueleza kuwa fedha hizo zilikuwa zikilipwa na Shirika la afya AMREF kwa ajili ya kazi ya kufuatilia kila mgonjwa lengo likiwa kuhakikisha hali zao za kiafya zinaimarika.

Alieleza baada ya kufuatilia na kujiridhisha iliitisha kikao  ca pamoja kilichohusisha ofisi ya mganga mkuu wilayani Muheza na wanaohusika kuhudumia watu wanaoishi na VVU pamoja na AMREF.

Akifafanua zaidi sababu zilizopelekea kwa watumishi hao kutokuwa waadilifu ni kutumiwa pesa moja kwa moja  kwa mhudumu kupitia simu yake ya mkononi na kwa kuweka takwimu hewa kwa lengo la kujiongezea posho.

Mkuu huyo wa TAKUKURU mkoani Tanga,alieleza kwamba baada hatua zilizochukuliwa  ni pamoja na kuitisha kiako cha pamoja kati ya Takukuru na ofisi ya mganga mkuu wa wilaya ya Muhuza  (DMO) na watendaji wake wote wanaohusika na kuhudumia watu wanaoishi na VVU pamoja na Amref.

Hata hivyo, alisema  katika kikao hicho Takukuru iwasilisha yaliyobainika katika ukaguzi kwa kuwatembelea  jumla ya zahati 7 katika 16 zilizopo wailayani Muheza  na kubaini kuwepo kwa tatizo hilo, ambapo   ilimuagiza  Mganga mkuu wa  Wilaya hiyo  kufanya uhakiki  wa Takwimuza wagonjwa wote wanaoishi na VVU  na kutoa taarifa za uhakiki.

“Baada ya agizo  hilo , ilibainika  kuwepo kwa jumla ya wagonjwa hewa 313, ambapo idadi hiyo ya wagonjwa hewa iliondolewa, na kupewa  barua za kujieleza  kwa kitendo caho  cha kusajiuli wagonjwa hewa , lakini wizara ya Afya imetoa maelekezo ya kufanyika uhakiki  kwa wateja wanaotumia dawa ambazo sio halisi.”alifafanua Bi Zainabu.

Hata hivyo,TAKUKURU Mkoa wa Tanga imetumia nafasi hiyo kuwasihi watumishi wa umma kufanya  kazi kwa kwa mujibu wa kanuni , taratibu , sheria  na miongozo iliyopo katika utekelezaji wa majukumu yao.

Mwisho.




 

No comments:

Post a Comment