NA SOPHIA WAKATI,TANGA
Mara baada ya kukabidhi hizo,Elizabeth amesema benk imegushwa na utendaji kazi wa jeshi la polisi kupambana na uhalifu kwa kutumia mashindano ya Ulinzi Cup kutoa elimu kwa vijana kujiepusha na kuwafichua wanaojihusisha na vitendo viovu.
Polisi Jamii
yaibuka Kidedea Ulinzi Cup.
TIMU ya Soka
Polisi Jamii FC yenye maskani yake FFU Majani mapana Jijini Tanga imefanikiwa kutoka kifua mbele baada ya kuifunga Tanesco kwa mabao 4 – 1 katika
mchezo wa Ligi ya kuwania Kombo la Ulinzi uliofanyika Uwanja wa shule ya msingi Kombezi.
Polisi jamii ilikuwa ya kwanza kufunga magoli yake kupitia vinara wa timu hiyo, Khalifa Hussein aliyeifungia mabao mawili dakika ya 11 na 47,huku Shauri Juma goli moja dakika ya 48, Salimu
Mazimu goli moja dakika 78 mpambano ambao ulikuwa na burudani ya kuvutia.
Goli la
kufutia machozi la Tanesco Tanga lilipachikwa kimiani na Mwedi aliyewahadaa
walizni wa Police Jamii na kuachia mkwaju mkali uliokwenda moja kwa moja wavuni
na kumsinda mlinda mlango Endrew Solnaj.
Kwa matokeo
hayo Police Jamii wamefanikiwa kuwa washindi watatu kwenye ligi hiyo iliyokuwa
ikishirikisha timu 20 huku ikiendeshwa kwa mtindo wa mtoano.
Lengo
la ligi hiyo ilikuwa ni Jeshi la Polisi
kushirikiana na Jamii hususani Vijana kupitia sekta ya michezo kutumia mpira wa
miguu kupambana na vitendo vya uhalifu.
Kwa kutumia
jukwaa hilo Jeshi la Polisi limekuwa likitoa elimu kwa Jamii kupambana na
uhalifu kwa kutoa taarifa za kuwafichua wahalifu ili sharia kuchukua mkondo
wake.
Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Tanga,Henry Mwaibambe katika mazungumzo yake na Wanahabari
alisema juzi kuwa,fainali za ligi hiyo zitafanyika baada ya kumalizika kwa
mashindano ya ngao ya hisani Jijini Tanga.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment