Sunday 6 August 2023

SIMBA DAY PONGWE ILIKUWA HIVI,,,WAPENZI NA WANACHAMA WA KLABU YA SIMBA WAGAWA MISAADA,,

Pichani ni miongoni mwa wapenzi na wanachama wa klabu ya Simba Pongwe mkoani Tanga Kuelekea Simba Day:wakifanya usafi wa mazingira kituo cha afya Pongwe na kugawa zawadi kwa wagonjwa wodi mbalimbali. 

NA SOPHIA WAKATI,TANGA

KATIKA kuelekea Simba Day Wapenzi na Wanachama wa Klabu ya Simba kutoka tawi la Pongwe Best lililopo nje kidogo ya Jiji la Tanga, wametoa misaada ya Kijamii kwa  kutoa zawadi mbalimbali ikiwa seemu ya kufariji wagonjwa waliolazwa kwenye Kituo cha afya Pongwe.

Misaada hiyo ni pamoja na Sabuni za unga na vipande huku wakitumia fursa hiyo kufanya usafi kwenye mazingira ya kituo hicho cha afya ambapo wana Simba hao wametumia siku ya jana kushirikiana na jamii.

Mbali na kufanya shughuli hiyo katika kituo cha afya Pongwe lkini pia wapenzi hao wa timu ya Simba wwaliwatembelea wazee wanaoishi kwenye Kambi ya watu wanaougua ugonjwa wa ukoma ya Umba.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Simba tawi la Pongwe Best, Patrice Mgendi alisema kwamba; “Tumeamua kutumia siku hii kuelekea Simba Day kuwafariji wagonjwa na wenye mahitaji maalum”alisema.

Asha Salmada ambaye ni mganga mfawidhi wa kituo cha afya Pongwe alisema kwamba, wamefarijika kuona wana Simba hao wamechukua hatua kuona umuhimu wa kuisaidia jamii jambo ambalo husaidia kuwapatia faraja.

“Kwa niaba ya Kituo, tumejisikia vizuri wana Simba kufanya usafi na kuwapa zawadi wagonjwa, tunaomba timu nyingine zingeiga mfano huu”alisema Salmada.

Wana Simba wengine walioshiriki zoezi hilo la kutoa zawadi kwa wagonjwa walisema kwamba, wamedhamiria utaratibu huo wa kuchangamana na jamii kuwa endelevu kwa kuwa wana wajibu kufanya hivyo kama watanzania.

Pamoja na hayo Salmada alitoa rai kwa wana Simba na wanamichezo wengine kuwa tayari kushiriki mazoezi mengine akitolea mfano lile la kuchangia damu sanjari na kutembelea kituo cha afya Pongwe kupima afya zao.

Mwisho.

 













 

No comments:

Post a Comment