NA SOPHIA WAKATI,TANGA
WAMILIKI
wa Mahoteli na Nyumba za kulala wageni Jijini Tanga wamesema, wamejipanga
vizuri katika kuwahudumia Wageni wanaofika kwa ajili ya shughuli mbalimbali
ambapo wameahidi kuwapatia huduma za kimsingi kama vile chakula aslia na hata
malazi bila kuwepo kwa usumbufu wa aina yeyote.
Meneja
mapokezi wa Hoteli ya Mtendele Hoteli iliyopo eneo la Chuda Jijini Tanga, Zaina
Mohamediamesema kwamba, katika utekelezaji wa majukumu yao,wamejipanga katika
utoaji wa huduma bora kwa wateja wao hatua ambayo lengo lake ni kuvutia wageni
zaidi kutembelea Tanga.
“Kiukweli
tumejipnga kuwahudumia vyema wateja wetu katika utoaji huduma zenye viwango vya
ubora na hata gharama zetu kuwa nafuu mkwa upande wa malazi na hata chakula
tunachoawapatia”alisema Mwakilishi huyo wa Hoteli ya Mtendele iliyopo maeneo ya
Chuda katika Halmashauri ya Jiji la Tanga.
Zaina alisema
kwamba, katika kutoa huduma hizo wamekuwa wakihakikisha wanapika chakula chenye
ubora huku malazi yakiwa katika kiwango kinachostahiki jambo ambalo wageni
wanaofika kupata huduma wamekuwa wakilifurahia wakati wote na hivyo kuwafanya
kuwa na wateja wa uhakika.
Alisema
kuwa, kwa mgeni anayefika Tanga, ataweza kufurahia chakula asilia
kilichotengenezwa katika mahadhi ya Pwani sanjari na meneo ya malazi kuwa
tulivu, safi na usalama ukiwa wa hali ya
juu ambapo amewato wasiwasi wateja wanaotembelea Jiji la Tanga kwamba
watakapofika watahudumiwa vyema.
“Kwa
kweli kwa upande wetu si watoa huduma za Hoteli Tanga tumejipanga vyema…Tanga
ni Jiji la aina yake.Mgeni atakapofikia kwenye Hoteli na Nyumba zetu za kulala
wageni atapata huduma ambazo hataweza kusahau, ubora wa vyakula na malazi ni wa
hali ya juu, tunapika chakula asilia”alisema Zaina.
Akizungumzia
mashindano ya ngao ya Hisani yanayoendelea kufanyika Jijini Tanga,Zaina alisema,licha
ya kuwepo kwa wageni wengi lakini wote wanahudumiwa katika viwango
vinavyostahiki na hivyo hakuna malalamiko kutoka kwa wateja wao huku
akisisitiza kusema Tanga ni shwari nwakati wote.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment