Thursday 19 October 2023

WASHIRIKI BONANZA LA NYERERE DAY 2023 WASHAURI MAKAMPUNI NA WAMILIKI VIWANDA KUJITOKEZA KUDHAMINI VILABU KUNUFAIKA NA KUJITANGA,,,,,,

Pichani ni kikombe kilichoshindaniwa katika bonanza la soka timu za veteran 2023 katika kumbukumbu ya kumuenzi baba wa taifa Mwalim Julius Kambarage Nyerere lililofanyika uwanja Popatlaly jijini Tanga.

NA SOPHIA WAKATI,TANGA

Bingwa mtetezi wa bonanza la kumuenzi Baba wa taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere 2022 amekiri kwamba mshindi Suka Veteran ya jijini Dar e salaam  aliyeshinda kwa kufunga magoli 7-6 kwa mikwaju ya penati amepatikana kihalali.

Kocha wa timu ya Kijichi veteran yenye masikani yake Mtoni kijichi wilayani Temeke jijini Dar es alaam,Lenus Mwegobwe ameyasema hayo mara baada ya kuisha pambano hilo la fainali.

Alisema kwamba wao ni washiriki na walijiandaa vizuri katika kundi lao la timu nne na kufanikiwa kushinda hatua ya awali na kufanikiwa kuingia hatua kucheza fainali kuhakikisha wanatetea ubingwa wao wa mwaka jana lakini bahati haikuwa yao.

Mashindano yaliandaliwa vizuri,wapinzani wetu Suka veteran walifanikiwa kuibuka bingwa kwa mikwaju ya penati 7-6 na  kuibuka kuwa mabingwa Nyerere Day mwaka 2023 jijini Tanga.

‘’Tunakubali matokeo ya mchezo wa fainal,tunaipongeza timu ya Mandingo veteran ya jijini Tanga waandaaji wa bonanza hilo,baada ya kukosa ushindi tunakwenda kujiandaa na mabonanza mengine.

Pia ametumia nafasi hiyo kuwashauri wachezaji wa vilabu vya veterani mbalimbali kujitokeza kwenye vilabu vyao ili kuweza kufanya mazoezi kujiweka vizuri kiafya na kushiriki mabonznza.

‘’Maviterani tunatakiwa kujiweka vizuri kiafya,pia kukutana kwenye mabonanza yanayofanyika mikoa mbalimbali kuweza kukutana na kubadilishana mawazo’’Alisema kocha wa Kijichi veteran Lenus.

Mwisho.  

Pichani ni Mwenyekiti wa timu ya soka Kitambi Noma veteran ya jijini Arusha, Jemes Rugangila  mara baada ya mchezo wa fainal umuhimu na faida za klabu za veterani zimebeba kundi kubwa wakiwemo watumishi na wafanyabiashara mbalimbali.

NA SOPHIA WAKATI,TANGA

WADAU wa bonanza la kumuenzi Baba wa Taifa Mwalim Julias Kambarage Nyerere wametumia fursa hiyo kuwashauri wachezaji wa zamani kujiunga na vilabu vya veteran ili waweze kutunza vipaji vyao na kujenga mtandao ndani na nje ya nchi.

Hata hivyo,amewashauri wawekezaji wa viwanda na makampuni mbalimbali kujitokeza kuweza kudhamini vilabu vya veteran ili kuweza kutumia sekita ya michezo kuweza kutangaza shughuli zao ndani na nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa timu ya soka Kitambi Noma veteran yenye maskani yake jijini Arusha, Jemes Rugangila  amesema mpira wa veteran umebeba kundi kubwa wakiwemo watumishi na wafanyabiashara na wakubwa.

Alisema kwamba kwa kupitia klabu ya Kitambi Noma veteran wamefanikiwa kujenga mtandao na klabu mbalimbali na ikiwemo Pars chini ya Muti veteran,Umoja zinazoundwa na wafakazi na wafanyabiashara wa nchini Kenya.

‘’Sisi Klabu ya kitambi Noma veteran ni washiriki wa kudumu kwenye mabonanza tuko chini ya Tanskim na mdhamini mkubwa TBL wamekuwa wakisapoti safari zetu kutembea Tanzania na nje ya nchi’’alisema Mwenyekiti huyo wa Kitambi Noma Jemes.

Alisema kwamba umoja huo wa vilabu vya veteran umebeba kundi kubwa watumishi wa serikali na wanyabiashara wakubwa na wadogo lengo kubwa kujenga urafiki wa kudumu kwa kutembeleana kupitia sekta hiyo ya michezo.

Akizungumzia zaidi ushiriki wao katika mabonanza ikiwemo la kumbukumbu kumuenzi baba wa taifa Mwalim Julias Kambarage Nyerere lililoandaliwa na timu ya Mandingo veteran ya jijini Tanga,lilikuwa zuri sana hatukuweza kuwa mabingwa lakini tunajiandaa na mashindano mengine.

‘’Kushiriki mabonanza ni utaratibu wetu wa kawaida,katika kundi letu bonanza la Nyerere Day tumecheza vizuri sana lakini hatukubahatika kuwa washindi,tunakwenda kujiandaa na bonanza jingine la Madesho Day linalo tarajiwa kufanyika mkoani Moshi.

‘’Mpira wa veteran umebeba kundi kubwa wengine wakiwa wafanyakazi,wafanyabiashara,wenye kufanya maamuzi kwenye makampuni,wenye zaidi ya miaka 35 ,hivyo wadhamini wanaweza kunufaika kutangaza biashara zao’’alisema Jemes.

Klabu ya Kitambi Noma veteran ya jijini Arusha ina mpango mkakati wa kuandaa mbio ya Marathon mwaka 2024 kwa kushirikisha vilabu mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Amesema mbio hiyo itakayofahamika kwa kwa Kitambi Noma Marathon 2024 itashikisha vilabu vyote vya veteran ndani na nje ya nchi lengo kuweza kufurahi,kuendeleza urafiki iliojengeka kupitia sekta ya michezo. 

Mwisho.   


NA SOPHIA WAKATI,TANGA

Msemaji wa Timu ya Suka Veterani ya Jijini Dar es salaam, Ramadhani Athumani Mganga ametamba kwamba, ubingwa walioupata umetokana na maandalinzi ya kujiandaa na bonanza hilo kutimiza ndoto yao

Hata hivyo,amesema ni kutokana na mkakati uliopo baina ya wachezaji na viongozi kushirikiana kuibuka kuwa bingwa msimu huu wa 2023 na kufungua milango kujiandaa na mabonanza mengine yatakayojitokeza ndani na nje ya nchi.

Msemaji huyo,Ramadhani maarufu Bufon alieleza kuwa tulifanya maadalinzi ya muda mrefu chini ya kocha Boban na ilikuwa ni dhamira yao ya dhati kuibuka kuwa washindi.

Aidha,amewapongeza waandaji Mandingo veterani ya jijini Tanga kuandaa bonanza hilo ambalo limesaidia kuwakutanisha kukumbushana na kubadilishana mawazo na kuweza kujenga mtandao.

''Suka veterani ni klabu ambayo inaongoza kujikusanyia makombe mengi kupitia mabonanza na niwashiriki wa kudumu na tutaendelea kujipanga''Alisema msemaji huyo wa Suka veterani Ramadhan huku akiwasihi wachezaji wenye vipaji vya soka kujitokeza kujiunga klabu za veterani.  

Aidha,alisema kwamba, kitu pekee wanachoweza kujivunia ni uwepo wa wachezaji mahiri wakiwemo wale walioweza kuwika vipindi vilivyopita.

“Sisi klabu ya Suka veteran tumekuwa na maandalizi toka mwaka jana, timu yetu inayoongoza kwa makombe mengi.Tunawapongeza walioamdaa Bonanza wenzetu wa mandingo veteran”

Alibaishani kuwa mara baada ushindi huo Kikosi kitaendelea kunolewa na Kocha wa Haruna Moshi maarufu ‘Bobani’kiukweli tumepata kombe tunawashukuru sana Mandingo veteran kwa kuandaa bonanza.

Hata hivyo,Msemaji huyo wa klabu ya Suka Veteran Ramadhan amesema Baada ya ushindi huo Suka Veteran wanakwenda kujiandaa mazoezi kuelekea Moshi kwa Bonanza na baadaye Arusha kwa mchezo kama huo.

Mwisho.




Pichani ni miongoni mwa wachezaji wa timu ya Suka veterani wakielekea jukwaani uwanja wa soka wa Popatlaly kwa ajili ya kuvishwa medani kabla ya kukabidhiwa zawadi za ushindi.

 

No comments:

Post a Comment