Thursday 29 August 2024

RIADHA TANGA KUMPA USHIRIKIANO MUANDAAJI WA MASHINDANO YA TANGA CITY MARATHON



Pichani ni Waandaaji wa Mashindano ya Tanga City Marathon wakionyesha medali ambazo zitatolewa kwa washiriki wa mbio hizo msimu huu

Na Sophia Wakati,Tanga.

CHAMA cha Riadhaa Mkoa wa Tanga (RT) kimesema kwamba kitampa ushirikiano wa kutosha muandaaji wa Mashindano ya Riadhaa ya Tanga City Marathon ili kuweza kuondoa changamoto zilizojitokeza msimu uliopita na yaweze kuwa na tija na mafanikio makubwa.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Chama cha Riadha (RT) Mkoani Tanga,Sophia Wakati alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari kuhusu namna walivyojipanga kuhakikisha wanampa ushirikiano wa kutosha muadaaji huyo ili mashindano hayo yaweze kufanyika kwa ufanisi.

Alisema pia kuweza kufanyika vizuri kwa kufuata taratibu zote za Mashindano hayo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga kupitia Afisa Michezo Mkoa

“Mbio hizi za Tanga City Marathon ni mashindano muhimu kwa mchezo wa Riadha mkoani hapa na kwa sasa tumeyaingiza kwenye kalenda ya Mkoa na sasa yatakuwa yakifanyika kila mwaka na sisi RT kwa kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga tutatoa ushirikiano wa kutosha kwa waandaaji”Alisema Sophia Wakati.

Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika Septemba 22 mwaka huu ambapo yataanzia kwenye Hotel ya Tanga Beach Resort na kuzunguka maeneo mbalimbali Jijini Tanga na kuishia hapo huku yakishirikisha wakimbiaji katika makundi matatu ya Kilomita 21,10 na 5 za kujifurahisha.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment